Ubaguzi wa kijinsia
hutokana na hali ya kupendelea jinsi moja na kunyima haki au stahiki jinsi
nyingine. Kwa mfano, ubaguzi huu unaweza kuwa katika utoaji wa huduma tofauti,
au haki tofauti ambazo hazizingatii misingi imara, ya ujenzi wa usawa kati ya
wanawake na wanaume. Katika jamii nyingi nchini, hali hii ya ubaguzi wa
kijinsia, hujitokeza kwa mfano katika ubaguzi wa muundo wa kijinsia dhidi ya
wanawake kuhusiana na mapato, ufikiaji wa huduma na raslimali na kushiriki
katika maamuzi nyeti yanayohusu maisha yao na ya kijamii.
No comments:
Post a Comment