Sunday, August 14, 2022

Ubaguzi wa Kijinsia.

 


Ubaguzi wa kijinsia hutokana na hali ya kupendelea jinsi moja na kunyima haki au stahiki jinsi nyingine. Kwa mfano, ubaguzi huu unaweza kuwa katika utoaji wa huduma tofauti, au haki tofauti ambazo hazizingatii misingi imara, ya ujenzi wa usawa kati ya wanawake na wanaume. Katika jamii nyingi nchini, hali hii ya ubaguzi wa kijinsia, hujitokeza kwa mfano katika ubaguzi wa muundo wa kijinsia dhidi ya wanawake kuhusiana na mapato, ufikiaji wa huduma na raslimali na kushiriki katika maamuzi nyeti yanayohusu maisha yao na ya kijamii.

No comments:

Post a Comment