Dhana ya 1: Jinsi na
Jinsia
Jinsi:
Kwa
kawaida, binadamu huzaliwa na jinsi ya kike au kiume. Jinsi hizi ni tofauti
za kibaologia tu. Tofauti hizi za
kibaologia hazina tabaka na hazihusiana na nani kati ya mwanamke au mwanaume ni
wa hali ya juu zaidi ya mwenzake. Hali
ya kuzaliwa ke au me (biologia)
haibadiliki. Hali hii ina majukumu yake (kama mfano, mwanamke hubeba mimba na
kunyonyesha na mwanamume hutunga mimba)
Jinsia: Ni dhana ambayo
hutumika katika kuelezea mahusiano ya kijamii yaliyojengeka kati ya mwanaume na
mwanamke. Dhana hii hutumika kuelezea tafsiri ya kijamii kuhusu maana ya kuwa
mwanamke au mwanaume, ikiwa inatoa utofauti katika thamani ya utu wao, stahiki
na haki zao pamoja na nafasi zao kama vile: wajibu au kazi, madaraka, maamuzi,
umiliki wa rasilimali n.k. Hivyo basi, dhana hii mara nyingi hutumika katika
kutoa tafsiri ambayo inaelezea mahusiano yanayooundwa na jamii, na ambayo huwa
nje ya tofauti za kibaolojia kati yao. Tafsri hii ya kijamii ambayo mara nyingi
huimarishwa na mifumo ya kidini, kielimu na kisera/bajeti, inaashiria
kumbebesha mwanamke wajibu mkubwa katika kuzalisha na kuendeleza kizazi na
nguvu kazi ya jamii husika na kumnyima haki sawa na hasa usawa wa kufikia na
kumiliki huduma za kijamii, raslimali za nchi, kufaidi matunda ya jasho lao
pamoja na ushiriki ulio imara katika maamuzi yanayogusa maisha ya jamii kutoka
ngazi ya familia, kitaifa na kimataifa. Vilevile wakati mwingine kuondoa utu na thamani ya
maisha yao kwa njia ya kuhalalisha au kuendeleza vitendo vya ukatili na
udhalilishaji dhidi yao. Kwa kuwa mahusiano haya yamesababisha pengo la kijinsia
yamejengwa na wanajamii (wa kiume na wa kike) yanaweza kubadilishwa na kuleta
usawa wa kijinsia yenye tija katika jamii (WFT: Kitita cha Mafunzo ya Rushwa ya
Ngono).
No comments:
Post a Comment