Thursday, August 18, 2022

Mchakato wa Mabadiliko Binafsi katika uongozi wa kifeminia

 

Mchakato wa Mabadiliko Binafsi katika uongozi wa kifeminia 

na deogratius Koyanga 

Makala ya Valerie Miller na VeneKlasen (2012) Imebainisha kanuni nne za kuzingatia kwenye mchakato wa mabadiliko binafsi kwa wanaharakati watetezi wa haki za wanawake. Katika harakati kuna uongozi, uongozi ili uwe na ufanisi na ulete mabadiliko, unahitaji mabadiliko binafsi ya kiongozi. Kiongozi awe na mtazamo chanya, abadilishe mtazamo wake wa awali kabla ya kuwa mwanaharakati, na pia aweke misingi ya kutaka kuona mabadiliko chanya yatakayosababishwa na yeye. kwahiyo hapa ni lazima abadilike.  Valerie na veneKlasen, wanandika hizi kanuni ambayo zitatusaidia kubadilika sisi kwanza: 

Kanuni ya Kwanza ni: Ujuzi na Ufahamu muhimu

Waandishi hawa wanadai kwamba elimu na maarifa ya itikadi ya ukombozi wa mwanamke inaanza kwenye maisha halisia ya mwanamke anayopitia kwenye safari ya mabadiliko.

Maarifa haya hayapatikani kwenye darasa rasmi, bali yanatokana na uzoefu unaoanza kwa kujiifunza kuhoji mambo yalivyo “kawaida” Mifano ya maswali ni kama haya

 

Mchakato wa kuanza kuhoji ubaguzi na mifumo kandamizi humjengea mwanamke yoyote ufahamu na hamasa kubwa ya kutamani mabadiliko .

Makala za Valerie Miller na VeneKlasen (2012) zimebainisha viwango vya ufahamu vinavyochochea wanawake na hasa viongozi kuchukua hatua za kudai na kufanya mabadilko wanapopata fursa ya kushika usukani wa uongozi.

 

Kanuni ya 2: Kuhakikisha na Kujenga Juu ya Ufahamu wa Wwanawake na Roho (Validating and building on women’s knowledge and spirit)

Katika safari ya kujenga uelewa na ufahamu binafsi, lazima mwanaharakati afike mahali ambapo anajenga imani na ile ajenda bila wasiwasi au mashaka. Kwenye ngazi hii kunahitajika wingi wa watetezi wenye   uelewa wa muktadha na mifumo kandamizi ili iimarishe uelewa na ufahamu (knowledge and consciousness raising). mambo ambayo yanawezesha kuhakikishia misimamo iliyochukuliwa na mielekeo ni pamoja na kusoma kumbukizi za wapambanaji, mashairi, nyimbo na sanaa zinazoimarisha uelewa kukuza hamasa  na kuhakikisha  misimamo ya binafsi na mielekeo.

Kanuni ya 3. Kuelewa na kutafakari suala la mamlaka (Understanding and navigating power).

Uwezo wa mwanaharakati kujenga uelewa wa jinsi mamlaka(nguvu) ndani ya jamii ya mfumo dume inavyofanya kazi ni nyenzo muhimu ya kumwezesha kuungana na wengine katika kujenga mikakati ya kuvunja hizi nguvu na kujenga njia mbadala ya kutumia nguvu zilizoko kwenye nafsi zao (power within)

Wachambuzi wa jinsi mamlaka (power) inavyofanya kazi ndani ya jamii wamebainisha njia mbili. Kwanza kwa njia inayoonekana (visible power), ikiwa ni pamoja na sheria, sera zinazohalalisha ubaguzi wa jinsia. Mamlaka au nguvu iliyojificha (invisible power) Wenye mamlaka kama viongozi wa dini, matajiri wa dunia na taasisi zinazowalinda kama Benki Kuu ya Kimataifa, Shirika la Biashara la Kmataifa,  vina uwezo wa kuumba? au kujenga ajenda za kisiasa zinazolinda maslahi yao. Kwa mfano sera za kubinafisisha huduma za jamii, sera za soko huria zote hizi zinalinda maslahi ya mabepari, zinawakandamiza maskini na mafukara wa dunia na kuwabebesha wanawake mzigo wa ziada kwenye shughuli za kuendeleza kizazi na nguvu kazi.

Uelewa wa jinsi nguvu hizi zinavyofanya kazi huwezesha mwanamke mmoja mmoja kuona umuhimu wa kuunganisha nguvu zake kujenga mshikamano wa kupambana na hizi nguvu kandamizi.

Kanuni ya 4 - Kujitunza (Moyo, akili-mwili) (Self-care - Heart-mind-body)

Afya ya kiongozi ni rasilimali kwake, kwa familia, kwa shirika au asasi anayoongoza na kwa tapo la utetezi wa haki za wanawake kimapinduzi. Mara nyingi shughuli za uanaharakati ni kazi inayotumia nguvu nyingi ya kimwili, kiakili,  kifikra na hata kiroho. Shughuli hizi ukiunganisha na shughuli nyingine za uzalishaji (productive) na za kuendeleza kizazi (reproductive) zinaweza ziwe na athari kubwa kwenye afya ya hisia (emotional health), afya ya mwili (physical health) na afya ya akili (mental health).Umuhimu wa kujali afya ni sehemu muhimu za uanaharakati  wa mapambano dhidi ya mifumo kandamizi..

 

Misingi Binafsi inayomwongoza kiongozi wa harakati za utetezi wa wanawake kimapinduzi

 

Ø    Hii inamaanisha kwamba, kiongozi wa harakati za ukombozi wa wanawake kimapinduzi ni yule mwenye kuamini na kuongozwa na  misingi ya usawa, na  ukombozi wa wanawake kimapinduzi.

 

Ø    Ni kiongozi anaehamisika na uelewa wa itikadi na mwenye utayari wa kujiimarisha kwenye uelewa huu ili aweze kujenga mazingira wezeshi ya kujifunza pamoja (shared learning).

Ø    Mwenye dhamira ya kuweka mifumo mibadala ya uongozi itakayowezesha ushiriki wa pamoja katika kujenga ajenda ya pamoja, kujadili, kuendeleza na kutetea ajenda ya ukombozi wa wanawake kimapinduzi.

Ø    Ni kiongozi mwenye dhamira, nia na uwezo wa  kuchambua hali halisi ya muktadha wa siasa na uchumi kwa kubainisha fursa na changamoto za kuendeleza harakati za utetezi wa haki za wanawake kimapinduzi.

Ø    Ni kiongozi mwenye uwezo wa kushirikiana na wenzake kubainisha mafanikio ya pamoja na mwenye utayari wa kuwajibika kutokana na makosa au mapungufu yatokanayo na maamzi ya pamoja (celebrate collective achievements and assume individual accountability on behalf of the collective).

Ø    Kiongozi mwenye uwezo na dhamira ya kujenga mahusiaono mbadala ndani ya shirika yenye kujali utu wa kila mmoja, wenye kusaidiana wakati wa shida na mwenye kutabiri viashiria vya kugawa nguvu za pamoja.

Ø    Ni kiongozi mwenye utayari wa kushikamana, kutandaa  na viongozi na mitandao yenye kuongozwa na misingi ya utetezi wa wanawake kimapinduzi kama mkakati wa ujenzi wa tapo la kusambaratisha mfumo dume.

Ø    Ni kiongozi mwenye upeo wa kuona mahusiano kati ya mfumo dume na mifumo mingine kandamizi inayotumia rangi, jinsi, tabaka, hali ya maumbile na ujinsia wa mtu kukandamiza na kuwabagua wanawake na watu waliko pembezoni.

Ø    Kiongozi mwenye dhamira na utayari wa kushirikiana na wengine katika kupambana na mifumo mingine kandamizi bila kupoteza ajenda ya ukobozi wa mwanamke kimapinduzi. 

Ø    Vilevile ni kiongozi mwenye nia na dhamira ya kushirikiana kwa kugawana majukumu na siyo kushindana.

Ø    Ni kiongozi anachukulia  cheo kama dhamana inayompa wajibu na siyo mamlaka ya kutawala na kumrisha.

Ø    Mwisho na siyo kwa daraja ni kiongozi mwenye kujali afya yake na ya wale anaowaongoza kama mkakati wa kujenga afya ya shirika na afya ya tapo.

Ø    Mwezeshaji ajumuishe akizingatia mwongozo wa Mkataba wa Kanini za Ukombozi wa Wanawake wa Kiafrika Kimapinduzi.

No comments:

Post a Comment