Ukombozi ni mchakato wenye kumwezesha mtu kujinasua kutoka
minyororo inayomnyima haki ya kujithamni na kuthaminiwa na wengine, haki ya
kuulindwa utu wake, haki ya kusikilizwa na kuzikiliza, haki ya kumiliki mwili
wake, haki ya kushiriki katika uongozi wa jamii yake, yaki ya kushiriki na
kufaidi matunda yatokanayo na jasho lake, haki ya kufikia na kunufaika
rasilimali ya taifa lake. Ukombozi wa mwanamke kimapinduzi ni hali na mchakato
uliyomwezesha mwanamke kujinasua kutoka minyororo ya mifumo kandamzi
inayombagua na kumsabilishia kukosa haki na stahiki sawa kama mwanaume.
Mchakato huu unaanza kwenye ngazi ya kujitambua na kukataa ubaguzi wa aina
yoyote, kukataa fikra mgando zinazohalisha ubaguzi wa jinsia, kujiunga na
wengine kwenye harakati za kusambaratisha mfumo dume.
No comments:
Post a Comment