Sunday, August 14, 2022

Dhana ya Ukombozi wa Mwanamke Kimapinduzi

 


Ukombozi ni mchakato wenye kumwezesha mtu kujinasua kutoka minyororo inayomnyima haki ya kujithamni na kuthaminiwa na wengine, haki ya kuulindwa utu wake, haki ya kusikilizwa na kuzikiliza, haki ya kumiliki mwili wake, haki ya kushiriki katika uongozi wa jamii yake, yaki ya kushiriki na kufaidi matunda yatokanayo na jasho lake, haki ya kufikia na kunufaika rasilimali ya taifa lake. Ukombozi wa mwanamke kimapinduzi ni hali na mchakato uliyomwezesha mwanamke kujinasua kutoka minyororo ya mifumo kandamzi inayombagua na kumsabilishia kukosa haki na stahiki sawa kama mwanaume. Mchakato huu unaanza kwenye ngazi ya kujitambua na kukataa ubaguzi wa aina yoyote, kukataa fikra mgando zinazohalisha ubaguzi wa jinsia, kujiunga na wengine kwenye harakati za kusambaratisha mfumo dume.  

No comments:

Post a Comment