Vyama vinane vya Siasa vyaanza mchakato wa kuandaa sera ya Jinsia
Na Deogratius Temba
VYAMA vinane (8) vya siasa nchini Tanzania vimekutana na kujadiliana namna ya kuanza mchakato wa kuandaa sera ya Jinsia ndani ya vyama vyao ili kuweka misingi ya kuwezesha ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi wa kisiasa.
Vyama hivyo ni Chama cha Kijamii (CCK), Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha ACT-Wazalendo, Chama cha Mapinduzi (CCM), ADA-TADEA, Chama cha Wakulima (AAFP), Alliance for Democratic Change (ADC), ambavyo vinaanza zoezi hili kwa awamu kama sehemu ya akutekeleza maazimio ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini Tanzania.
Mchakato huu unaendeshwa kwa kuwezeshwa na wataalam wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Shirika la Sheria na Maendeleo Afrika (WiLDAF), ambao wanatekeleza mradi wa uwezeshaaji Wanawake kushiriki katika vyombo vya maamuzi na uongozi na siasa.
Kwa mujibu wa Baraza la Vyama vya siasa, Mpango wa awamu ya kwanza ya mchakato huu utavihusu vyama hivyo vinane vilivyoteuliwa kwa kufuata orodha ya Mpangilio wa kiherufi (A-Z) na baadaye vitafuata vyama vilivyobaki.
Tayari timu za wawezeshaji zimeshapangwa kwaajili ya kushiriki mchakato huo ndani ya vyama ambao unatarajiwa kuanza mapema wiki ijayo, na baadaye rasimu za sera za Jinsia kwa vyama hivyo vinane zitawasilishwa katika Baraza la Vyama vya siasa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa kwaajili ya utekelezaji na ufuatiliaji.
Mwisho
Na Deogratius Temba
VYAMA vinane (8) vya siasa nchini Tanzania vimekutana na kujadiliana namna ya kuanza mchakato wa kuandaa sera ya Jinsia ndani ya vyama vyao ili kuweka misingi ya kuwezesha ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi wa kisiasa.
Vyama hivyo ni Chama cha Kijamii (CCK), Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha ACT-Wazalendo, Chama cha Mapinduzi (CCM), ADA-TADEA, Chama cha Wakulima (AAFP), Alliance for Democratic Change (ADC), ambavyo vinaanza zoezi hili kwa awamu kama sehemu ya akutekeleza maazimio ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini Tanzania.
Mchakato huu unaendeshwa kwa kuwezeshwa na wataalam wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Shirika la Sheria na Maendeleo Afrika (WiLDAF), ambao wanatekeleza mradi wa uwezeshaaji Wanawake kushiriki katika vyombo vya maamuzi na uongozi na siasa.
Kwa mujibu wa Baraza la Vyama vya siasa, Mpango wa awamu ya kwanza ya mchakato huu utavihusu vyama hivyo vinane vilivyoteuliwa kwa kufuata orodha ya Mpangilio wa kiherufi (A-Z) na baadaye vitafuata vyama vilivyobaki.
Tayari timu za wawezeshaji zimeshapangwa kwaajili ya kushiriki mchakato huo ndani ya vyama ambao unatarajiwa kuanza mapema wiki ijayo, na baadaye rasimu za sera za Jinsia kwa vyama hivyo vinane zitawasilishwa katika Baraza la Vyama vya siasa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa kwaajili ya utekelezaji na ufuatiliaji.
Mwisho





No comments:
Post a Comment