Monday, November 13, 2023

WILDAF Conducts Gender Mainstreaming Training for Forum CC Staff

By- Our Reporter in Dodoma

The Women in Law & Development in Africa (WILDAF) conducted a capacity-building training for the staff of the Climate Change Forum (Forum CC) to integrate gender issues into the organization's programs and structures. 


Participants in a group photo after the day one session


 This training is part of a broader project funded by the Sida through Save the Children aimed at strengthening organizational capacity, enhancing institutional structures, and amplifying the voices of children to discuss, advocate for, and assert their fundamental rights, particularly in the realm of climate change. The joint initiative is being implemented by WILDAF, Forum CC and 5 other consortium partners.  



During the training conducted by WiLDAF, Forum CC Executive Director, Sarah Ngoy, highlighted the significance of the workshop in the context of a gender gap identified within the organization during a capacity assessment conducted in 2022. She emphasized the need for capacity-building among staff to ensure gender responsiveness in programs and advocated for systemic changes to address gender equality issues comprehensively.

Deogratius Temba, a facilitator from WiLDAF


Ngoy expressed gratitude for the insights gained through the training and outlined specific areas for improvement. These include making budgets gender-responsive, increasing training for staff, allocating a budget for sanitary pads for female employees, providing a resting room for pregnant mothers, and revising financial guidelines to cover costs for assistants to breastfeeding women and assistants of people with disabilities.

Post-training, the organization plans to conduct a thorough review of internal policies and guidelines, including the human resources policy, to align them with the organization's gender policy. Ngoy announced the development of a gender implementation plan scheduled to commence in 2024.

Deogratius Temba, the facilitator from WILDAF, expressed optimism regarding the potential for significant institutional changes following the training. He highlighted the participants' commitment to contributing to institutional change, ensuring that all activities within the organization become gender-responsive.








WiLDAF yafanya mafunzo ya Usawa wa Kijinsia kwa Forum CC

Na Deogratius Temba, Dodoma

 Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WILDAF),imefanya mafunzo ya kujenga uwezo kwa wafanyakazi wa Jukwaa la Mabadiliko ya tabia nchi (Forum CC), ili kuweza kuingiza masuala ya Kijinsia katika Programu na muundo wa shirika kwa ujumla.
Washiriki wa Mafunzo ya Jinsia, ambao ni wafanyakazi wa FORUM CC wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mafunzo, na Mwezeshaji kutoka WiLDAF, Deogratius Temba

Mafunzo hayo, ambayo ni sehemu ya mradi wa kukuza uwezo wa asasi za kiraia, kuimarisha mifumo ya kitaasisi na kuongeza sauti za watoto kujadili, kujisimamia na kudai haki zao za msingi hasa katika eneo la Mabadiliko ya tabia nchi, unaotekelezwa na WILDAF na Forum CC.
Majadiliano wakati wa warsha ya Jinsia iliyowezeshwa na WiLDAF  
Akizungumza katika mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Forum CC, Sarah Ngoy, amesema kwamba, mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi huo, ambapo mwaka jana 2022, taasisi hiyo ilifanya zoezi la kupima uwezo wake katika masuala ya Kijinsia na kuonekana kwamba kuna pengo kwenye eneo la usawa wa Kijinsia ndani ya taasisi.
Mwezeshaji akisisitiza Jambo wakati wa warsha ya Uingizwaji wa masuala ya Kijinsia kwenye Taasisi, iliyofanywa na WiLDAF kwa Forum CC

“warsha hii kwa wafanyakazi wetu imekuja kwa wakati muafaka, mwaka jana tulipofanya zoezi la kujipima kama taasisi tuliona hili pengo la kijinsia ndani ya shirika, tukagundua kwamba pamoja na kuhitaji kujenga uwezo kwa wafanyakazi wetu kwenye masuala ya Kijinsia, ili kuzifanya program zetu ziwe na mtazamo wa Kijinsia, pia tulihitaji mabadiliko ya kimfumo, sambamba na kuongeza uelewa na maarifa ya masuala ya kijinsia kwa timu yetu yote”alisema Sarah na kuongeza: “Warsha hii imetufungua macho sana, kumbe bado tuna pengo la masuala ya kijinsia, kumbe tunahitaji kufanya mabadiliko na maboresho ya bajeti zetu ziweze kuwa na mtazamo wa kijinsia, kupitia mafunzo haya tumegundua kwamba tunatakiwa kuongeza mafunzo kwa wafanyakazi, kuweka bajeti kwaajili ya taulo za kike kwa wafanyakazi, kuweka chumba cha kupumzika mama wajawazito wanapokuwa ndani ya shirika letu, na pia kubadilisha mwongozo wa fedha ili kuruhusu kuwalipia gharama wasaidizi wa wanawake wanaonyonyesha na wasindikizaji wa watu wenye ulemavu” alisema Sarah.
Wafanyakazi wa Forum CC wakifuatilia warsha

Ameongeza kwamba, mara baada ya mafunzo hayo, taasisi hiyo itakaa na kupitia upya sera za ndani ya shirika na miongozo mbalimbali ukiwemo ule wa rasilimali watu ili uweze kuendana na sera ya Jinsia ya Taasisi sambamba na kuwa na mpango wa utekelezaji wa masuala ya Kijinsia kwa taasisi utakaoanza kutekelezwa mwaka 2024. Naye mwezeshaji kutoka WiLDAF, Deogratius Temba, amesema kwamba, WiLDAF
Mwezeshaji, Deogratius Temba, akisisitiza mabadiliko ya Kitaasisi kwa mtazamo wa Kijinsia, wakati wa mafunzo ya Jinsia kwa wafanyakazi wa Forum CC

inamatumaini kwamba, baada ya mafunzo hayo, mabadiliko makubwa ya kitaasisi yatatokea kwani washiriki wameweka ahadi (commitiment) ya kuweka nguvu kwenye mabadiliko ya kitaasisi ili kila kitu kinachofanyika ndani ya shirika kiweze kuwa na mtazamo wa Kijinsia.


Tuesday, November 7, 2023

Miaka 30 ya TGNP: Tanzania kinara utekelezaji wa maazimio ya Beijing

 

na Deogratius Temba

Makamu wa Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini, Dkt. Phumzile Mlambo Ngcuka,  amesema T
anzania inaongoza katika kutekeleza maazimio ya Mkutano wa nne wa wanawake duniani uliofanyika Beijing Nchini china mwaka 1995.

Mgeni wa Heshima katika tamasha la Jinsia la 15, Makamu wa Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini, Dkt. Phumzile Mlambo Ngcuka



Akizungumza wakati wa sherehe za ufunguzi wa Tamasha la Jinsia la 15,  na miaka 30 ya ya Mtandao wa Jinsia Tanznaia (TGNP), Mhe. Phunzile ambaye amekuwa pia Mkurugenzi Mkuu wa Shirika linaloshughulikia masuala la Wanawake (UNwomen),  ambaye alikuwa mgeni rasmi, alisema kwamba, Mkutano wa Bijing uliofanyika miaka 28 uliweka maazimio ambayo Tanzania imeendelea kufanya vizuri kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na nchi nyingine.



“Kwa uelewa wangu wa kufanya kazi katika ngazi ya kimataifa, ninaweza kuona mchango wa TGNP katika kujenga uwezo kwa wanawake wa Tanzania kufanya uchambuzi wa masuala ya Kijinsia, ni nchi ya Kolombia na Tanzania pekee ambazo wanawake wamejenga uwezo kwa kiasi kikubwa wa kiuchamnganuzi na kiuchambuzi kuhusu masuala ya Kijinsia.” Alisema na Kuongeza kwamba



“Mkutano wa Beijing uliipa Tanzania heshima kubwa Zaidi, ukizingatia kwamba uliongeozwa na Mtanzania ambaye aliweka historia ambayo haitasahaulika duniani kwakuwa mkutano ule ulizaaa maazimio amzito kabisa ambayo yamesababisha mageuzi wa kimifumo, kisera na kisheria katika mtataifa mbalimbali lakini pia maazimio yale yamepelekea kuongeza vuguvugu la harakati hizi kuanzia ngazi ya jamii hadi kitaifa, na sasa kuna misamiati mingi ya kukomboa wanawake…”



Aliongeza kwamba, dunia itaendelea kuikumbuka Tanzania kwa kile kilichotokea Beijing, chini ya uongozi wa Balozi Getrude Mongela, ambapo hata hivyo nchi inaongoza kwa kuwa na sera zenye mtazamo wa Kijinsia ikiwepo mabadiliko ya kisheria na kimwongozo.

Kwa  upande wake Mkurugenzi Mkaazi wa UNWomen Tanzania,  akitoa salaam, alisema kwamba Changamoto za mapengo ya usawa wa Kijinsia bado zipo, ikiwepo Ukatili wa Kijinsia, lakini  kunahitajika nguvu ya mapoja na mshikamano wa mashirika mbalimbali ili kutokomeza kabisa vitendo vya Ukatili wa Kiinsia.



“tusipofanya jitihada za ziada, itachukua Zaidi ya miaka 300 kufikia usawa wa Kijinsia, tunahitaji kujipanga, kushikamana, kuwahusisha wanawake na wanaume kwa umoja wao ili kuzuia mabaya yote ambayo wanawake na watoto wa kike na kiume wanatendewa” alisema Odan.



Awali alitoa hotuba yake Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi alisema kwamnba, Tamasha linatoa fursa ya wana jamii hususan wanawake kushirikishana uzoefu, kujadili, kujifunza, kujenga ajenda ya pamoja kuhusu usawa wa jinsia na maendeleo hususani ya namna ya kupanga mikakati ya pamoja ili kusonga mbele kwa pamoja.



“Tunaposheherekea mafanikio ya harakati zetu kwa miaka 30 ya uwepo wa TGNP, hatuna budi kuipongeza serikali kwa kukubali maoni na mapendekezo kadhaa mbayo tumekuwa tukipelekea na haya ndio yamesababisha Tanzania kuonekana kwamba imetekeleza kwa kiasi kikubwa maazimio ya Beijing…” alisema Lilian.  



Friday, October 27, 2023

Viti Maalum vifutwe- Mtandao wa Wanawake, Katiba na Uongozi


Na Deogratius Temba

 

Mtandao wa Wanawake, Katiba, Uongozi na Uchaguzi, ambao wamekuwa wakidai na kushawishi mabadiliko ya kisera, kisheria na kimuundo ili kutoa nafasi sawa kwa wanawake kushiriki kwenye nafasi za uongozi katika nyanja mbalimbali wametoa msimamo wao juu ya uwepo wa Viti Maalum katika nafasi za uongozi wa kisiasa.

Wawakilishi wa Mtandao wa Wanawake, Katiba, Uongozi na Uchaguzi, wakiwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ofisini kwake Ikulu Dar es salaam, wakati akiwa Makamu wa Rais. (Picha na Maktaba yetu)


Mara baada ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuteua Kikosi Kazi cha kukusanya maoni na kuyachakata juu ya namna ya kukuza Demokrasiasa nchini, Kikosi kazi ilichofanya kazi chini ya Uenyekiti wa Prof. Rwekaza Mkandala,  pamoja na kwamba Mtandao waliwasilisha maoni yao kwa kikosi kazi, moja ya pendekezo lao kama msimamo ni kuhusu muundo wa Viti maalum vya Ubunge, udiwani na Halmashauri za Vijiji na Kamati za Mitaa unaotumika hivi sasa.

Wanamtandao wa Wanawake, Katiba, Uongozi na Uchaguzi ni muunganiko wa asasi za kiraia zaidi ya 200 ulioanzishwa mwaka 2011, ulishauri kwamba mfumo wa Viti Maalum uliopo sasa ufutwe katika ngazi zote za uongozi.  Kwa mantiki hiyo, kusiwepo na Viti Maalum vya wanawake.

Katika Mapendekezo ya Mtandao, wanasema kwamba: “ Licha ya kwamba, wadau walishauri kuondolewa kwa mfumo wa Viti Maalum, Kikosi Kazi kiliamua Mfumo wa Viti Maalum uendelee bila kutoa sababu za msingi za kuendeleza huu mfumo” inaeleza sehemu ya Taarifa ya Mapendekezo ya Mtandao wa wanawake na Katiba na kuongeza kuwa:

“Kikosi Kazi kilipendekeza kwamba, Wabunge wa Viti Maalum waitwe Wabunge wa Taifa na Madiwani waitwe Madiwani wa Wilaya. Vile vile Kikosi Kazi kilipendekeza Sheria ya Mfuko wa Uchaguzi ibadilishwe ili Wabunge wa Viti Maalum wafaidike nao kama Wabunge walioteuliwa kwa kupitia majimbo ya Uchaguzi. Na kwamba kuweko kwa mwongozo wa kisheria wa uteuzi wa wagombea na uchaguzi wa viongozi ndani ya Vyama vya Siasa ikiwemo wabunge wa Viti Maalum ili kusaidai uteuzi na uchaguzi wa haki na huru” pendekezo hili la Kikosi kazi, Mtandao unalikataa.

Mtandao wa wanawake na Katiba hawakubaliani pia  na maoni ya Kikosi kazi kwamba;  mfumo wa viti maalum uliopo sasa uendelee kutumika kama njia ya kupata uzoefu na kisha kupisha wanawake wengine wenye nia ya kuongeza uzoefu na ujuzi wa masuala ya siasa,

“ Kwetu sisi Wanamtandao wa Wanawake, Katiba, Uongozi na Uchaguzi, tunaona pendekezo la kuendeleza Viti Maalum ambavyo sisi kama wadau tunaoathirika na mfumo huu uliopo ambao tunaona umejaa ubaguzi na udhalilishaji wa Kijinsia, tunashauri ubadilishwe au kuondolewa kabisa” inasema sehemu ya Mapandekezo ya Mtandao.

 

Lakini pia, wanamtandao wa wanawake Katiba, Uongozi na Uchaguzi, wanasema kwamba,  kuendeleza mfumo wa Viti Maalum wa sasa ni kuijengea jamii Imani kwamba, wanawake bado hawana uwezo, uzoefu, wala ujuzi wa masuala ya siasa, na kwamba  wengi ikiwa ni pamoja na hao walioko kwenye uwanda wa siasa tayari, kwamba wanahitaji takriban miaka kumi ya kujenga uwezo huo ili kuwapisha wengine wanaowania kuingia kwenye uwanda wa siasa.

 

Ni muhimu kujenga fikra chanya kuhusu uwezo wa wanawake, na pia kutokuwaunganisha kwenye kapu moja na Makundi Maalum. Wanawake sio wote ni makundi maalum kwa sababu hata wanaume baadhi yao wapo kwenye kundi maalum.

 

Tafsiri ya Mtandao wa wanawake, Katiba Uongozi na Uchaguzi juu ya kuendeleza mfumo wa Viti Maalum, ni la kuturudisha nyuma, na kupuuza hazina ya ujuzi, uwezo  ulioko miongoni wa wanawake wengi kwenye masuala ya siasa na uongozi.

 

Nchi yetu inatakiwa kuweka mazingira salama, wezeshi na kuondoa vikwazo kwenye michakato ya uchaguzi ili kuwapa nafasi wanawake washindane na wanaume. Tunapoelekea kwenye chaguzi za serikali za Mitaa mwaka 2024, ni muhimu kuanza kujiandaa kuweka mifumo rafiki ya uchaguzi kwa wanawake ili wagombee na wanaume, na wapigiwe kura ambazo sio za huruma au za kupewa kwa sababu wao ni wanawake.

Ili kushughulikia usawa wa kijinsia katika uongozi, serikali ilifanya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka za Serikali za Wilaya (1982) na marekebisho Na.4 ya mwaka 2000 katika kifungu cha 35 ili kuanzisha jitihada za makusudi za kuongeza uwakilishi wa wanawake katika serikali za mitaa ambapo wanawake wanapaswa kufikia theluthi moja ya wajumbe wa mabaraza.

 

Katika ngazi ya kijiji, wanawake wanapaswa kuwa asilimia 25 ya wajumbe wa Halmashauri ya kijiji ambayo kwa kawaida ina wajumbe 15 hadi 25. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa asilimia 30 ya viti maalum kwa wanawake Bungeni na asilimia 33.3 ya viti maalum katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Ingawa mafanikio makubwa yamepatikana, Serikali bado haijafikia lengo la Umoja wa Afrika la usawa wa kijinsia wa 50/50.

Tuesday, October 24, 2023

AZAKI zajadili Tekonolojia na Usawa wa Kijinsia


Na deogratius Temba, Arusha

ASASI za zimejadili namna ambavyo ni vigumu kutenganisha mabadiliko ya Sayansi na Tekonolojia na Usawa wa Kijinsia kwa maendeleo endelevu.




Akizungumza, wakati wa ufunguzi wa Wiki ya AZAKI nchini inayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa (AICC) Jijini Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Asasi za Kiraia (FCS), Francis Kiwanga alisema kwamba jamii haiwezi kukwepa kwenda sambamba na mabdiliko ya sayansi na Teknolojia ikiwepo kulinda na kuheshimu haki za Binadamu na usawa wa kijinsia.  



“mwaka huu tunakutana hapa, Zaidi ya AZAKI 500, mijadala yetu yote itajikita katika kujadili, Tekonolojia na Jamii, wapi tumetoka, Tulipo, na tunapokwenda. Tusigope, mabadiliko ni makubwa sana, kasi ya mabadiliko haikwepeki” alisema Kiwanga na Kuongeza:

“Miaka ya 2000, watu waliogopa sana, walifikiri, ujio wa komputa utafuta ajira zote, makatibu muhutasi walifikiri hawatakuwepo tena na wataondoka, lakini hadi leo wao..”




Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) ni moja ya wadau wanaoshiriki Mkutano huo,pia ni wajumbe wa Kamati ya Maandalizi, na watatoa mada  na kujenga mjadala juu ya Ubunifu wa Kiteknolojia kama chachu ya Usawa wa Kijinsia.



Katika warsha hiyo ya TGNP pia watakuwepo wadau muhimu ambao ni Taasisi ya Teknolojia ya Dar es salaam (DIT) ambao wanafunzi wa kike watapata nafasi ya kuonesha mashine walizotengeneza zinazolenga kupunguza gharama za matibabu kwa jamii 

TGNP,DIT waendesha majadala wa Usawa wa Kijinsia katika Tekonolojia

Na Mwandishi Wetu, Arusha #CSOWEEK2023 

 Wadau wamatakiwa kondoa hofu na mabadiliko ya Sayansi na kiteknolojia katika utendaji wa shughuli za kila siku ili kupunguza gharama za uendeshaji na uzalishaji.
Kaimu Mkuu wa Idara ya Ushawishi na Utetezi (TGNP), Florah Ndaba, akitoa maelezo wakati wanafunzi wa Chuo cha DIT wakielezea Mashine za kusaidia kupumua walizotengeneza. 

Hayo yameibuka kwenye mjadala ulioendeshwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) katika, uliowakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta binafssi, serikalini, wanazuoni na asasi za kiraia, katika wiki ya AZAKI #WIKIYAAZAKI2023 inayoendelea katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa (AICC) Jijini Arusha, ambapo pamoja na mengine, ujumbe mkuu ulikuwa ni ubunifu na Teknolojia kama chachu ya usawa wa Kijinsia.
Mwezeshaji kutoka TGNP akitoa maelezo ya awali juu ya ubunifu wa wasichana katika Sayansi na Tekonolojia ili kutatua changamoto za Jamii

Akizungumza wakati wa jopo, Kaimu Mkuu wa Idara ya Ushawishi na Utetezi, TGNP Florah Ndaba alisema kwamba, Jamii haipaswi kuogopa wala kuwa na hofu juu ya ukoaji wa teknolojia badly ni kuangalia, teknolojia isitumike bibaya kuongeza Ukatili na udhalilishaji wa Kijinsia au kuongeza tofauti za kiuchumi kati ya wanawake na wanaume.

 “Teknolojia, inapunguza gharama za utendeshaji na uzalishaji, Ndio maana TGNP tuliingia makubaliano ya DIT kusaidiana katika kuendeleza kuhakikisha jitihada za ubinifu wa kisayansi zinazofanywa na DIT zinazingatia usawa wa Kijinsia lakini pia wasichana wanaochagua fani za sayansi na tknolojia wanapata nafasi na kulelewa vipaji vyao hadi waingie kwenye soko la ajira” alisema Flora Naye Mwanajopo mtaalamu na Mchambuzi wa Masuala ya Kijinsia Deogratius Temba, alisema kwamba, kukosekana kw a usawa wa Kijinsia katika teknolojia kunaikosesha nchi fedha nyingi ambazo zingepatikana kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji.
Wana jopo mara baada ya Mjadala Wanafunzi wa Chuo cha DIT na Mkufunzi wao na Timu kutoka TGNP

 “ Utafiti uliofanywa na UNwomen kwa nchi 51 mwaka 2022, umeeleza kwamba, nchi za uchumi wa chini na Kati ambazo hakuna usawa wa Kijinsia katika Teknolojia zinapoteza Dola za Kimarekani Trilion 1 kila mwaka, na ifikapo mwaka 2025, zitapoteza Zaidi ya dola za kimarekani Trilion 1.5. Ukiangalia hii ni kwamba, Usawa wa Kijinsia kwenye eneo la Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati hauepukiki” alisema Temba.


 Aidha, akizungumza Mkufunzi kutoka Taasisi ya Tekonolojia Dar es salaam, (DIT), Nizentha Kimario, alisema kwamba DIT imekuwa na mtazamo wa Kijinsia, mahusiano yake na TGNP yamesaidia pia kujenga uelewa wa masuala ya Kijinsia na kubadili mitazamo hasi juu ya uwezo wa wasichana katika fani za sayansi na Teknolojia, lakini pia kwamba wanafunzi wanaona umuhimu wa kwenda kwenye jamii kuangalia changamoto na mahitaji yao kabla ya kuanza kufanya ubunifu. 





 “utaona kwamba, mashine nyingi za kibunifu tumebuni kutokana na mahitaji ya jamii. Wanafunzi wetu baada ya kuona kuna changamoto ya gharama kubwa ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo ndio walikuja na mashine hii hapa, lakini pia kuna gharama kubwa kwenye kutunza na kuwawekea dawa watoto wenye changamoto ya kupumua hasa arthima, ndio maana vijana wetu tena wasichana wamebuni hii mashine..” alisema Kimario. Sambamba na mijadala huo, wanafunzi kutika Chuo cha DIT walionesha mashine mbalimbali ambazo zimebuniwa na wanafunzi, na Pikipiki ya magurudumu matatu (Bajaji) yenye uwezo wa kubeba abiria saba (7) na Dereva ambayo inatumia nishati ya Betri la kuchaji. Wiki ya AZAKI 2023 inayoratibiwa na Mfuko wa Asasi za Kiraia (FCS), imeanza Oktiba 23 hadi 27 2023 jijini Arusha ikiwa imewahusisha wakurugenzi, wafanyakazi na wadau mbalimbali wa asasi za kiraia Zaidi ya 500, wadau wa maendeleo, wataalamu kutoka serikalini na wanajamii ambao wananufaika na rasilimali na kazi za AZAKI.

Sunday, October 22, 2023

TGNP kushiriki wiki ya CSO Arusha, kuonesha ubunifu wa wasichana wa DIT

 

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) inashiriki maadhimisho ya wiki ya Asasi za Kiraia (CSO) inayofanyika Jijini Arusha kwa kutoa elimu juu ya umuhimu ya wajamii kushiriki kwenye ubunifu wa kisayansi na Kiteknolojia kwa kuzingatia usawa wa Kijinsia kwa maendeleo Endelevu.

Mkutano wa wahandishi wa Habari na Kamati ya Maandalizi ya Wiki ya CSOs uliofanyika leo jijini Arusha

Maadhimisho ya Wiki ya CSOs yanayotarajiwa kuanza kesho Oktoba 23, 2023 Jijini Arusha yatahusisha asasi za kiraia Zaidi ya 500, kutoka  mikoa yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nchi jirani, huku kukiwa na mada mbalimbali ambapo mada kuu inalenga ushiriki wa asasi za kiraia katika Teknolojia katika kufanikisha shughuli zake za kitoa huduma kwa jamii nchini,  na Zaidi kutafakari mafanikio ya nyuma, ya sasa na ya baadaye  sambamba na changamoto zake.

Akizungumza Mwakilishi wa TGNP katika Mkutano na wandishi wa Habari leo uliowahusisha wakurugenzi wa mashirika mbalimbali na kamati ya kitaifa ya uandaaji wa maadhimisho hayo, Deogratius Temba, alisema kwamba, pamoja na TGNP kushiriki kwenye shughuli zote, kwa kushirikiana na mashirika mengine, pia wataendesha warsha na majadiliano ambayo yataangazia Ubunifu na uvumbuzi  wa kiteknolojia kama chachu ya usawa wa Kijinsia.

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi na  Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Prof. Preksedis Ndomba, katika hafla ya makubaliano ya kushirikiana kukifanya chuo hicho kuwa Kitovu cha Jinsia, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wasichana wanapewa kipaumbele katika ubunivu katika Teknolojia (Picha na maktaba)


Temba ameeleza kwamba, mada hiyo itawahusisha wadau mbalimbali, mashirika, wanazuoni na wataalamu wanawake  na wasichana walio kwenye Ubunifu na uvumbuzi wa kiteknolojia katika kuondoa changanmoto zinazoikumba jamii hasa wanawake na watoto.

“Tutakuwa na wanafunzi wasichana kutoka DIT ambao ni wavumbuzi wa kiteknolojia, wanaolenga kuondoa changamoto za kijamii katika taifa letu. TGNP tumejenga uwezo kwa jamii na taasisi mbalimbali kubomoa mifumo kandamizi na mitazamo hasi juu ya uwezo na ushiriki wa wanawake hasa wasichana katika Sayansi, Teknolojia, na Hisabati, sasa wapo wasichana wanaofanya vizuri kwenye ngazi ya vyuo vikuu kama Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam (DIT), wamefanya vizuri sana,” alisema Temba na kuongeza:

“Ukiangalia kwa hapa tulipofikia kama nchi, tumepiga hatua, vifaa vipo,lakini bado kuna pengo la usawa wa kijinsia na ushiriki au ujumishwaji wa makundi yote, tunachofanya kwa kushirikiana na Taasisi mbalimbali ni kubadilisha mitazamo hasi, lakini pia kushaiwshi serikali kutenga bajeti ya kutosha kwenye TEHAMA hasa mashuleni, na kuondoa au kuunguza kodi kwa vifaa hivyo ili watoto waweze kujifunza na kuonesha ubunifu wao” alisema Temba.        

Aidha, amesema kwamba, Nchi kama Tanzania zinaweza kufaidika sana na kuendeleza sera na mipango inayowezesha ushiriki wa wanawake katika sekta ya teknolojia na kuhakikisha kwamba teknolojia inatumika kwa njia inayolinda usawa wa kijinsia. Hii inaweza kuchangia katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kuboresha hali ya maisha kwa wanawake na wanaume kwa usawa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi  ya wiki ya CSO Niensia Mahenge alisema kwamba, Teknolojia inatoa  fursa kwa wasichana na wanawake kupata elimu na kukuza ujuzi. Majukwaa ya kujifunza mtandaoni, programu za elimu, na rasilimali za kidijitali huwezesha kujifunza kwa umbali na kujifunza bila shinikizo la muda, kupunguza vikwazo vya kuingia.

“Teknolojia inaweza kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wanawake, hasa katika maeneo yasiyopewa kipaumbele. Huduma za tiba kwa njia ya mtandao na programu za afya za simu hutoa zana kwa wanawake kudhibiti afya na ustawi wao, ikiwa ni pamoja na huduma za ujauzito, uzazi wa mpango, na usaidizi wa changamoto za kiafya” alisema Mahenge.

Hata hivyo, wadau wameshauri kwamba  ni muhimu kuzingatia kuwa teknolojia na uvumbuzi pia yanaweza kuwa na athari hasi kwa usawa wa kijinsia ikiwa haitazingatia changamoto za kijinsia na inaweza kuongeza pengo la kidijitali. Kwa mfano, wanawake wengi katika nchi za dunia ya tatu wanaweza kukosa upatikanaji wa vifaa vya teknolojia au elimu ya kutosha ya kidijitali. Kwa hiyo, juhudi zinahitajika ili kuhakikisha kwamba teknolojia na uvumbuzi unawafikia wanawake na wanaume sawa na kuchangia katika kuboresha usawa wa kijinsia.

 

 

Monday, October 2, 2023

TGNP organized female leaders and their spouses to narrate success stories

 

Our Reporter, Kondoa

The Tanzania Gender Networking Programme (TGNP), in collaboration with the Aga Khan Foundation (AKF-T), has conducted a workshop on storytelling for female leaders and their spouses to discuss the challenges they face in fulfilling their leadership responsibilities.

Women Leaders and their spouses during the StoryTelling session held at Riverside Cottage, Kondoa


The workshop involved female councillors and their spouses, as well as leaders from wards, villages, and sub-villages in the Kondoa District Council in Dodoma Region.

Speaking, TGNP facilitator Deogratius Temba said that the project aims to build and strengthen relationships between leaders and their spouses while also addressing the challenges faced by female leaders on their journey towards development.

Storytelling facilitator, Mr. Deogratius Temba, during the session 


"Every leader present here has achieved success, and these successes have come through challenges as well. To reach a good state, there have been people who have enabled you to get there, perhaps your spouse, neighbor, teacher, party leader, employer, religious leader, or anyone else. But your story will build understanding for others and inspire them," said Temba.

He added that through storytelling, councilors will encourage female leaders from grassroots levels like sub-villages and villages to move forward. These areas often present significant obstacles related to customs, traditions, negative perceptions, and unpaid care work that weigh heavily on female leaders and hinder them from effectively fulfilling their leadership duties.

Hon. Fatma Idd Said the special Seat Councilor, Kondoa TC narrates her leadership journey


Sharing her story of facing obstacles and succeeding in her leadership journey, Fatuma Iddi Issa, a Special Seats Councilor in the Kondoa Town Council, explained that despite starting her political journey at the age of 20, she didn't achieve her goal at the expected time due to obstacles from people close to her.

"I was supposed to go far; if I hadn't been held back, I would be a Member of Parliament today, not just a councilor. But I lost my way in the middle. I haven't given up; I'm moving forward with confidence," said Fatuma.

Through discussions and storytelling, the spouses of female leaders also narrated their spouses' leadership journeys and how they helped them fulfill their leadership responsibilities by assisting with household chores such as child-rearing, meal preparation, fishing, farming, and livestock care.

In the storytelling of their leadership journeys by the attending female leaders, their spouses provided testimony on how they contributed to their wives' achievements. This included persuasion, financial empowerment, providing resources, and giving them time to fulfill their leadership duties.

TGNP yawezesha viongozi wanawake na wenza wao kusimulia hadhithi za mafanikio

 TGNP yawezesha viongozi wanawake na wenza wao kusimulia hadhithi za mafanikio

Na Mwandishi Wetu

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Aghakan Foundation (AKF-T), wameendesha warsha ya Masimulizi ya hadithi za mafanikio kwa viongozi wanawake na wenza wao ili kujadili changamoto wanazokumbana nazo katika kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi.  

Picha ya pamoja ya viongozi wanawake na wenza wao baada ya warsha iliyofanyika katika Ukumbi wa Riverside, mjini Kondoa


Warsha hiyo iliwahusisha Madiwani wanawake na wenza wao, viongozi wa Kata, vijiji na Vitongoji katika Halmashauri ya wilaya ya Kondoa, Mkoani Dodoma.

Akizungumza Mwezeshaji kutoka TGNP, Deogratius Temba, alisema kwamba Mradi huo unalenga kujenga na kuimarisha mahusiano kati ya wenza wa viongozi wenyewe lakini  pia kuangalia changamoto ambazo wanawake viongozi wanapitia hadi kufikia maendeleo.


“Kila kiongozi aliyepo hapa anayo mafanikio, mafanikio haya yamekuja kwa kupitia changamoto pia, kufikia hali nzuri kuna watu wamekuwezesha kufika hapo, labda ni Mwenza wako, jirani, mwalimu, kiongozi wa Chama chako, mwajiri, kiongozi wa dini au yeyote. Lakini pia hadithi yako itajenga uelewa kwa wengine na kuwatia moyo…’ alisema Temba


Washiriki wakiwa tayari kwa kusikiliza masimulizi ya hadithi za safari ya uongozi kutoka kwa viongozi wanawake


Ameongeza kwamba, kupitia masimulizi ya hadithi, madiwani watawapa moyo viongozi wanawake wanaotoka ngazi za chini vitongoji na vijiji ili wasonge mbele zaidi kwani huko ndiko wanakumbana na vikwazo vikubwa vya mila, desturi, mitazamo hasi, lakini pia majukumu ya kazi ambazo hazina malipo (unpaid care work)  yanawaelemea sana wanawake sana wanawake viongozi na kupelekea kushindwa kutekeleza vizuri majukumu ya kiuongozi.

Akitoa hadithi ya kukwama na kufanikiwa katika safari ya uongozi, Fatuma Iddi Issa Diwani wa Viti maalum, Halmashauri ya Kondoa Mji, alisema kwamba, pamoja na kuanza mapema safari ya kisiasa akiwa na umri wa miaka 20, hakufanikiwa  kufikia lengo lake kwa wakati kutokana na kukwamishwa na watu wa karibu.

Mhe. Fatma Said Idd, Diwani wa Viti Maalum, Kondoa Mji


“Nilitakiwa kuwa mbali sana, kama nisingekwamishwa, leo nilitakiwa kuwa Mbunge na sio Diwani tena, lakini nilipoteza mwelekeo  hapo katikati, sijakata tamaa, nasonga mbele kwa ujasiri “ alisema Fatuma.

Kupitia mjadala na masimulizi ya hadithi, wenza wa viongozi wanawake nao walisimulia safari za uongozi za wenza wao na jinsi ambavyo wamewawezesha kutimiza majukumu ya kiuongozi kwa kuwasaidia baadhi ya kazi za nyumbani kama kulea watoto, kuandaa chakula, kuvua, kusafisha shamba na kutunza mifugo.

Mwezeshaji kutoka TGNP, Deogratius Temba


Katika simulizi za safari ya uongozi kwa viongozi wanawake waliohudhuria, wenza wao walitoa ushuhuda jinsi ambavyo walichangia wake zao kufikia hatua hiyo, ikiwepo, kuwashawishi, kuwawezesha kifedha, rasilimali nyigine lakini pia kuwapa muda wa kutekeleza majukumu. 

Thursday, September 28, 2023

Men's Safe Space to discuss gender, masculinity, and women's leadership,

 

By Deogratius Koyanga, in Kondoa

The Gender Network in Tanzania (TGNP), in collaboration with the Aga Khan Foundation (AKF-(T)), through the "SHE LEADS" project in the Kondoa District Council in Dodoma Region, has organized a Safe Space Dialogue involving some male partners of women leaders in the Haubi Ward, starting from the ward level, villages, and hamlets.












Facilitating the dialogue, Deogratius Temba from TGNP stated that the aim of the dialogue is to change negative perceptions, customs, and traditions regarding women's participation in leadership positions and to enhance the collaboration of partners in improving the effectiveness of leaders in office.


He added that there is a need for male partners of women leaders to assist their spouses with some of the responsibilities traditionally associated with women, thereby reducing the workload on female leaders and enabling them to carry out their leadership roles for the benefit of the nation, bringing productivity and honour to female leaders.

"Many women face a heavy burden of family responsibilities that could be shared with their husbands or partners. However, the negative perception of women's leadership capabilities starts at the family level, and this significantly affects their performance. Customs, traditions, and religious beliefs strongly contribute to perpetuating this situation," said Temba.


Contributing to the discussion, some male participants shared provocative images and mentioned that women leaders at the ward, village, and hamlet levels face various challenges related to the intersection of family and leadership responsibilities.

Concluding the dialogue, the participants emphasized that men should be ready to help their wives with household duties, support their needs, build self-confidence in their roles, and abandon male-dominated systems.


Haubi Ward consists of four villages: Haubi, Mwisanga, Mafai, and Ntomoko. Among these, only Haubi Village has eight hamlets and three female hamlet chairpersons. However, women in village councils face significant challenges in balancing leadership duties and family responsibilities, such as fetching water and taking care of their families.

 

TGNP yaendesha Mjadala wa 'Nafasi Salama' kwa wenza wa viongozi wanawake

 

 

Na Mwandishi wetu, Kondoa

Mtandao wa Kijinsia Nchini (TGNP) kwa kushirikiana na Mfuko wa Aghakan(AKF-T) kupitia mradi wa ‘’SHE LEADS’’(Mwanamke Ongoza) kwenye Halmashauri ya Wilaya Kondoa Mkoani Dodoma, imeendesha Mjadala wa nafasi salama ‘safe space’ na baadhi ya Wanaume wenza wa Viongozi wanawake wanaotoka katika vitongoji na vijiji vya kata ya Haubi .








Akiongoza mjandala huo mwezehaji kutoka TGNP, Deogratius Temba, amesema lengo la mjadala huo ni kubadilisha Mtazamo,Mila na Desturi hasi kuhusu Ushiriki wa Wanawake kwenye nafasi za Uongozi na kuongeza ushirikiano wa wenza katika kuongeza ufanisi kwa viongozi walioko madarakani.

Ameongeza kuwa kuna kila haja ya wanaume wenye wake viongozi kuwasaidia wake zao  baadhi ya majukumu ambayo yamezoeleka ni ya wanawake hasa ya kijinsia ili kuwapunguzia viongozi wanawake mzigo wa kazi na kuwawezesha kutekeleza majukumu ya kiuongozi kwa manufaa ya Taifa na kuleta tija na heshima kwa viongozi wanawake.

“wanawake wengi, wanakabiliwa na mlundikano wa majukumu mazito ya kifamilia, ambayo yangeweza kufaywa na wanaume au wenza wao. Lakini pia, mtazamo hasi juu ya uwezo wa wanawake kuongoza unaanzia kwenye ngazi ya familia, hii ina athiri kwa kiasi kikubwa utendaji wao, Mila na desturi, misimamo ya kiimani inachochea sana kurudisha nyuma hii hali” alisema Temba.


Wakichangia mjadala baadhi ya Washiriki(wanaume) kupitia Picha chokoziwamesema wanawake viongozi ngazi ya kata,vijiji na vitongoji wanakumbwa na changamoto mbalimbali zinazohusiana na mwingiliano wa majukumu ya Kifamilia pamoja na Uongozi

Wakihitimisha mjadala huo washiriki hao wamesema wanaume wanapaswa kuwa tayari kuwasaidia wake zao majukumu ya nyumbani,kuwapa ushirikiano kupitia mahitaji yao ,kuwajengea uwezo wa kujiamini wanaposhiriki kwenye majukum yao pamoja kuachana na tabia ya mifumo dume.

Kata ya Haubi, ina vijiji Vinne ambavyo ni Haubi, Mwisanga, Mafai na Ntomoko, kati ya hivyo, kijiji cha Haubi pekee chenye vitongoji vinane (8) ndio vina wenyeviti wa vitongoji wanawake watatu (3). Lakini pia, wanawake walioko katika Halmasahuri za vijiji wanakumbana na changamoto kubwa ya kuacha majukumu ya kiuongozi na kutumia muda mwingi kwenye shughuli za kifamilia kama kutafuta maji na kuhudumia familia.