Na Mwandishi
wetu, Kondoa
Mtandao wa Kijinsia Nchini (TGNP) kwa
kushirikiana na Mfuko wa Aghakan(AKF-T) kupitia mradi wa ‘’SHE LEADS’’(Mwanamke
Ongoza) kwenye Halmashauri ya Wilaya Kondoa Mkoani Dodoma, imeendesha Mjadala wa
nafasi salama ‘safe space’ na baadhi ya Wanaume wenza wa Viongozi wanawake
wanaotoka katika vitongoji na vijiji vya kata ya Haubi .
Akiongoza mjandala huo mwezehaji
kutoka TGNP, Deogratius Temba, amesema lengo la mjadala huo ni kubadilisha
Mtazamo,Mila na Desturi hasi kuhusu Ushiriki wa Wanawake kwenye nafasi za
Uongozi na kuongeza ushirikiano wa wenza katika kuongeza ufanisi kwa viongozi
walioko madarakani.
Ameongeza kuwa kuna kila haja ya wanaume
wenye wake viongozi kuwasaidia wake zao baadhi ya majukumu ambayo yamezoeleka ni ya
wanawake hasa ya kijinsia ili kuwapunguzia viongozi wanawake mzigo wa kazi na
kuwawezesha kutekeleza majukumu ya kiuongozi kwa manufaa ya Taifa na kuleta
tija na heshima kwa viongozi wanawake.
“wanawake wengi, wanakabiliwa na
mlundikano wa majukumu mazito ya kifamilia, ambayo yangeweza kufaywa na wanaume
au wenza wao. Lakini pia, mtazamo hasi juu ya uwezo wa wanawake kuongoza
unaanzia kwenye ngazi ya familia, hii ina athiri kwa kiasi kikubwa utendaji
wao, Mila na desturi, misimamo ya kiimani inachochea sana kurudisha nyuma hii
hali” alisema Temba.
Wakichangia mjadala baadhi ya Washiriki(wanaume) kupitia Picha chokoziwamesema wanawake viongozi ngazi ya kata,vijiji na vitongoji wanakumbwa na changamoto mbalimbali zinazohusiana na mwingiliano wa majukumu ya Kifamilia pamoja na Uongozi
Wakihitimisha mjadala huo washiriki
hao wamesema wanaume wanapaswa kuwa tayari kuwasaidia wake zao majukumu ya
nyumbani,kuwapa ushirikiano kupitia mahitaji yao ,kuwajengea uwezo wa kujiamini
wanaposhiriki kwenye majukum yao pamoja kuachana na tabia ya mifumo dume.
Kata ya Haubi, ina vijiji Vinne
ambavyo ni Haubi, Mwisanga, Mafai na Ntomoko, kati ya hivyo, kijiji cha Haubi
pekee chenye vitongoji vinane (8) ndio vina wenyeviti wa vitongoji wanawake
watatu (3). Lakini pia, wanawake walioko katika Halmasahuri za vijiji
wanakumbana na changamoto kubwa ya kuacha majukumu ya kiuongozi na kutumia muda
mwingi kwenye shughuli za kifamilia kama kutafuta maji na kuhudumia familia.
No comments:
Post a Comment