Tuesday, November 7, 2023

Miaka 30 ya TGNP: Tanzania kinara utekelezaji wa maazimio ya Beijing

 

na Deogratius Temba

Makamu wa Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini, Dkt. Phumzile Mlambo Ngcuka,  amesema T
anzania inaongoza katika kutekeleza maazimio ya Mkutano wa nne wa wanawake duniani uliofanyika Beijing Nchini china mwaka 1995.

Mgeni wa Heshima katika tamasha la Jinsia la 15, Makamu wa Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini, Dkt. Phumzile Mlambo Ngcuka



Akizungumza wakati wa sherehe za ufunguzi wa Tamasha la Jinsia la 15,  na miaka 30 ya ya Mtandao wa Jinsia Tanznaia (TGNP), Mhe. Phunzile ambaye amekuwa pia Mkurugenzi Mkuu wa Shirika linaloshughulikia masuala la Wanawake (UNwomen),  ambaye alikuwa mgeni rasmi, alisema kwamba, Mkutano wa Bijing uliofanyika miaka 28 uliweka maazimio ambayo Tanzania imeendelea kufanya vizuri kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na nchi nyingine.



“Kwa uelewa wangu wa kufanya kazi katika ngazi ya kimataifa, ninaweza kuona mchango wa TGNP katika kujenga uwezo kwa wanawake wa Tanzania kufanya uchambuzi wa masuala ya Kijinsia, ni nchi ya Kolombia na Tanzania pekee ambazo wanawake wamejenga uwezo kwa kiasi kikubwa wa kiuchamnganuzi na kiuchambuzi kuhusu masuala ya Kijinsia.” Alisema na Kuongeza kwamba



“Mkutano wa Beijing uliipa Tanzania heshima kubwa Zaidi, ukizingatia kwamba uliongeozwa na Mtanzania ambaye aliweka historia ambayo haitasahaulika duniani kwakuwa mkutano ule ulizaaa maazimio amzito kabisa ambayo yamesababisha mageuzi wa kimifumo, kisera na kisheria katika mtataifa mbalimbali lakini pia maazimio yale yamepelekea kuongeza vuguvugu la harakati hizi kuanzia ngazi ya jamii hadi kitaifa, na sasa kuna misamiati mingi ya kukomboa wanawake…”



Aliongeza kwamba, dunia itaendelea kuikumbuka Tanzania kwa kile kilichotokea Beijing, chini ya uongozi wa Balozi Getrude Mongela, ambapo hata hivyo nchi inaongoza kwa kuwa na sera zenye mtazamo wa Kijinsia ikiwepo mabadiliko ya kisheria na kimwongozo.

Kwa  upande wake Mkurugenzi Mkaazi wa UNWomen Tanzania,  akitoa salaam, alisema kwamba Changamoto za mapengo ya usawa wa Kijinsia bado zipo, ikiwepo Ukatili wa Kijinsia, lakini  kunahitajika nguvu ya mapoja na mshikamano wa mashirika mbalimbali ili kutokomeza kabisa vitendo vya Ukatili wa Kiinsia.



“tusipofanya jitihada za ziada, itachukua Zaidi ya miaka 300 kufikia usawa wa Kijinsia, tunahitaji kujipanga, kushikamana, kuwahusisha wanawake na wanaume kwa umoja wao ili kuzuia mabaya yote ambayo wanawake na watoto wa kike na kiume wanatendewa” alisema Odan.



Awali alitoa hotuba yake Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi alisema kwamnba, Tamasha linatoa fursa ya wana jamii hususan wanawake kushirikishana uzoefu, kujadili, kujifunza, kujenga ajenda ya pamoja kuhusu usawa wa jinsia na maendeleo hususani ya namna ya kupanga mikakati ya pamoja ili kusonga mbele kwa pamoja.



“Tunaposheherekea mafanikio ya harakati zetu kwa miaka 30 ya uwepo wa TGNP, hatuna budi kuipongeza serikali kwa kukubali maoni na mapendekezo kadhaa mbayo tumekuwa tukipelekea na haya ndio yamesababisha Tanzania kuonekana kwamba imetekeleza kwa kiasi kikubwa maazimio ya Beijing…” alisema Lilian.  



No comments:

Post a Comment