Thursday, April 3, 2025

Tafakari ya Msamaha wakati wa Kwaresma


 

MSAMAHA NI NINI?

Msamaha ni uamuzi wa kuachilia hisia za hasira, chuki, na chuki dhidi ya mtu aliyekuumiza. Ni kuchagua kutokubali kwamba kosa la mtu huyo litakuwa na nguvu juu ya maisha yako, ni kuchagua kutokuendelea kutazama nyuma ambako mtu alikutendea uovu au kukwamisha mafanikio yako.

Msamaha ni kitendo cha kuacha kuudhika, kuachilia mtu aliyekukosea, na kuamua kutochukua kisasi. Ni uamuzi wa kuachilia maumivu ya moyo na hasira ambayo yamesababishwa na matendo ya mtu mwingine. Msamaha sio tu unawafungulia wengine, bali pia unawafungulia yule anayesamehe kutoka katika minyororo ya chuki na uchungu.

KWANINI TUNALAZIMIKA KUSAMEHE?

Ukibeba glasi au vikombe vya udongo kwenye kapu au mfuko ni lazima vigongane, kukwaruzana, kusuguana, na vingine kupasuka. Vikombe vinafanana sana na mfumo wetu wa maisha. Maisha ya binadamu yamejengwa kwenye harakati za kukutana, kuhusiana na kufanya kazi kwa pamoja, kufurahi pamoja, kuhuzunika pamoja nk. Katika harakati hizo, ndipo zinatokea hitilafu na migongano na migogoro ambapo inasabaisha makasiriko, chuki, hasira na kukoseana. Sasa basi, baada ya kukutana na hali hii, msamaha una maana gani kwetu?

  • Msamaha sio kusahau kwamba mtu alikukosea. Ni kukubali kwamba tukio hilo limetokea na kuchagua kuachilia maumivu yanayosababishwa nalo.
  • Msamaha hasa unakuhusu wewe. Ni njia ya kuponya na kusonga mbele.
  • Msamaha sio tukio la wakati mmoja. Ni mchakato ambao unaweza kuchukua muda. Wakati Fulani huchukua miezi, miaka nk.
  • Kusamehe haimaanishi kwamba unakubali tabia mbaya ya mtu mwingine.
  • Kusamehe kunaweza kuwa nguvu ya kubadilisha maisha. Inaweza kukusaidia kupata amani ya akili na uhusiano bora na wengine.

Msamaha ni zawadi unayojipatia mwenyewe

Ikiwa unakabiliwa na ugumu wa kusamehe, unaweza kutaka kuzungumza na mshauri,mshauri wa kiroho,  mchungaji, padre, Imam /mwalimu wa dini au mtaalamu wa afya ya akili. Wanaweza kukusaidia katika mchakato wa kupona. Hali hii inasaidia kukufanya utoke kwenye kifungo cha kubeba mzigo wa watu.

Umuhimu wa Kusamehe Watu Waliotukosea

Kusamehe ni zawadi kubwa tunayojipatia wenyewe. Inaweza kuwa vigumu sana, hasa pale tulipojeruhiwa sana. Lakini faida zake ni nyingi sana na zinaboreshesha maisha yetu kwa njia nyingi. Unaposamehe unatua mzigo, lakini unajipa furaha na Amani. Unaposamehe unaongeza fursa za kufanikiwa Zaidi, unapata Baraka kutoka kwa Mungu, “Utusamehe sisi, kama tulivyowasamehe wengine” ukisamehe unakuwa na afya njema, unapata nguvu za kuzalisha Zaidi kipato, kipato chako kinaongezeka mara dufu. Ukisamehe unakuwa na uwezo wa kuwasilisiliana vizuri na wateja wako na kuongeza uwezo wa kuuza na kununua na kujitengenezea uchumi bora. Msamaha una mafanikio makubw akw aliyeumizwa na kudsamehe kuliko aliyekosa.

Kwa nini ni muhimu kusamehe?

  • Chuki na hasira zinaweza kuleta mzigo mzito moyoni. Kusamehe ni kama kuondoa mzigo huo na kupata amani ya akili.
  • Kusamehe kunaweza kuboresha uhusiano wetu na wengine, hata na wale waliotutenda mabaya.
  • Uchungu wa kutokusamehe unaweza kuathiri afya yetu ya kimwili na kiakili, ukisababisha matatizo kama vile usingizi mbovu, mkazo, na hata magonjwa.
  • Katika dini nyingi, kusamehe ni sehemu muhimu ya ukuaji wa kiroho. Inatuunganisha zaidi na Mungu au nguvu ya juu zaidi. Mfano wakatoliki wanaashwa kusamehe kabla ya kupokea Ekaristi, lakini pia kabla ya kutoa sadaka yako, nenda kapatane na ndugu  yako.
  • Tunaposamehe, tunaonyesha wengine jinsi ya kushughulikia maumivu na kuchagua upendo badala ya chuki. Ukisamehe unaongeza ufanisi katika shughuli zako za kila siku, uhuru wa akili na nafsi, unakupa nguvu mpya na ubunifu katika utendaji

Jinsi ya kusamehe:

Kusamehe si jambo rahisi, lakini kuna hatua unaweza kuchukua:

  • Elewa hisia zako na kwa nini umejerahiwa.
  • Kushiriki hisia zako na mtu unayemwamini kunaweza kukusaidia kupata mtazamo mpya.
  • Kuandika juu ya hisia zako kunaweza kukusaidia kuzipanga vizuri.
  • Ikiwa unaamini katika Mungu, omba nguvu ya kusamehe.
  • Kila mtu hufanya makosa.

Kumbuka: Kusamehe sio sawa na kusahau. Ni juu ya kuchagua kuachilia maumivu na kusonga mbele.

 

Maandiko Matakatifu Yanasemaje Kuhusu Msamaha?

Maandiko Matakatifu, hususan Biblia, yanasisitiza sana umuhimu wa msamaha. Yesu Kristo, katika mahubiri yake Mlimani, alisisitiza kwamba tunapaswa kusamehe wale wanaotukosea, kama vile Baba yetu wa mbinguni anavyotusamehe sisi (Mathayo 6:14-15).

  • Mathayo 6:14-15: “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.”  
  • Marko 11:25-26: “Nanyi kila msimamapo na kusali, sameheni mkiwa na neno juu ya mtu, ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini msipowasamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.”  
Yesu alienda mbali zaidi kwa kufundisha kwamba tunapaswa kusamehe hata mara sabini na saba (Mathayo 18:21-22). Hii inaonyesha kwamba msamaha sio jambo la kufanya mara moja tu, bali ni mchakato unaoendelea katika maisha yetu

makala hii imeandaliwa na Deogratius Temba, Mwezeshaji, Mtafiti na Mchambuzi wa masuala ya Kijinsia, Tanzania-0784686575

No comments:

Post a Comment