Tuesday, October 24, 2023

AZAKI zajadili Tekonolojia na Usawa wa Kijinsia


Na deogratius Temba, Arusha

ASASI za zimejadili namna ambavyo ni vigumu kutenganisha mabadiliko ya Sayansi na Tekonolojia na Usawa wa Kijinsia kwa maendeleo endelevu.




Akizungumza, wakati wa ufunguzi wa Wiki ya AZAKI nchini inayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa (AICC) Jijini Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Asasi za Kiraia (FCS), Francis Kiwanga alisema kwamba jamii haiwezi kukwepa kwenda sambamba na mabdiliko ya sayansi na Teknolojia ikiwepo kulinda na kuheshimu haki za Binadamu na usawa wa kijinsia.  



“mwaka huu tunakutana hapa, Zaidi ya AZAKI 500, mijadala yetu yote itajikita katika kujadili, Tekonolojia na Jamii, wapi tumetoka, Tulipo, na tunapokwenda. Tusigope, mabadiliko ni makubwa sana, kasi ya mabadiliko haikwepeki” alisema Kiwanga na Kuongeza:

“Miaka ya 2000, watu waliogopa sana, walifikiri, ujio wa komputa utafuta ajira zote, makatibu muhutasi walifikiri hawatakuwepo tena na wataondoka, lakini hadi leo wao..”




Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) ni moja ya wadau wanaoshiriki Mkutano huo,pia ni wajumbe wa Kamati ya Maandalizi, na watatoa mada  na kujenga mjadala juu ya Ubunifu wa Kiteknolojia kama chachu ya Usawa wa Kijinsia.



Katika warsha hiyo ya TGNP pia watakuwepo wadau muhimu ambao ni Taasisi ya Teknolojia ya Dar es salaam (DIT) ambao wanafunzi wa kike watapata nafasi ya kuonesha mashine walizotengeneza zinazolenga kupunguza gharama za matibabu kwa jamii 

No comments:

Post a Comment