Na deogratius Temba, Arusha
ASASI za zimejadili namna ambavyo ni vigumu kutenganisha
mabadiliko ya Sayansi na Tekonolojia na Usawa wa Kijinsia kwa maendeleo
endelevu.
Akizungumza, wakati wa ufunguzi wa Wiki ya AZAKI nchini inayofanyika
katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa (AICC) Jijini Arusha, Mkurugenzi Mtendaji
wa Mfuko wa Asasi za Kiraia (FCS), Francis Kiwanga alisema kwamba jamii haiwezi
kukwepa kwenda sambamba na mabdiliko ya sayansi na Teknolojia ikiwepo kulinda
na kuheshimu haki za Binadamu na usawa wa kijinsia.
“mwaka huu tunakutana hapa, Zaidi ya AZAKI 500, mijadala
yetu yote itajikita katika kujadili, Tekonolojia na Jamii, wapi tumetoka,
Tulipo, na tunapokwenda. Tusigope, mabadiliko ni makubwa sana, kasi ya
mabadiliko haikwepeki” alisema Kiwanga na Kuongeza:
“Miaka ya 2000, watu waliogopa sana, walifikiri, ujio wa
komputa utafuta ajira zote, makatibu muhutasi walifikiri hawatakuwepo tena na
wataondoka, lakini hadi leo wao..”
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) ni moja ya wadau
wanaoshiriki Mkutano huo,pia ni wajumbe wa Kamati ya Maandalizi, na watatoa mada na kujenga mjadala juu ya Ubunifu wa
Kiteknolojia kama chachu ya Usawa wa Kijinsia.
Katika warsha hiyo ya TGNP pia watakuwepo wadau muhimu ambao
ni Taasisi ya Teknolojia ya Dar es salaam (DIT) ambao wanafunzi wa kike watapata
nafasi ya kuonesha mashine walizotengeneza zinazolenga kupunguza gharama za
matibabu kwa jamii
No comments:
Post a Comment