Friday, September 30, 2022

Wazazi NABA wahimizwa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili wa Kijinsia

 

Na Mwandishi Wetu

KUTOKANA na kuongezeka kwa vitendo vya Ukatili wa Kijinsia katika Jamii, hasa kwa watoto wanapokuwa nje ya shule, Jamii imeashwa kuwalinda watoto wa kike na kiume wanaotarajiwa kuahitimu darasa la saba mapema mwezi Oktoba mwaka huu.

Pia wazazi wameaswa kuhakikisha wakati wahitimu wa darasa la saba wakisubiria kuijunga na kidato cha kwanza mwakani, wanawaandalia watoto sehemu salama ya kuendelea kujifunza  na kuongeza maarifa ya kitaaluma au kuboresha vipawa na vipaji vyao Zaidi.

Akizungumza wakati wa mahafali ya nane ya shule ya awali na msingi ya NABA iliyopo Kata ya Saranga, manispaa ya Ubungo, jijini Dar es salaam, Diwani wa kata ya Saranga Edward Laizer ambaye alikuwa mgeni rasmi, alisema kwamba, wanafunziz wanaohitimu wamekuwa salama na kufikia kuhitimu darasa la saba akwa sababu waalimu walikuwa  makini, na walishirikiana vizuri na wazazi.

“Nina waasa sasa kuendeela kuwa karibu na hawa watoto, bado hawajawa watu wazima, wanatakiwa kuendelea kulelewa kimaadili, wanahitakiwa kuwa chini ya uangalizi, kuhitimu kwao leo tusiwache waka anza kuzurura mitaani, wakajiunga na vikundi vya uhalifu”.alisema Laizer katika hotuba yake.

 Aliongeza kwamba, Vijana wakikosa uangalizi, ndio tunapata changamoto ya watoto wa mitaani, panya road na makundi mengine ambayo yanaibuka katika jamii.

“Tunawasihi sana miezi hii ya kusubiria matokeo, tuwatafutie hawa vijana sehemu ya kukaa, vitu vya kufanya, kujifunza, ili wawe bize badala ya kuzurura mitaani. Zipo fursa za kujifunza computer, ufundi wa muda mfupi, kujifunza stadi za maisha, ambavyo pia vitawafanya watambue vipaji vyao” aliongeza

Laizer aliongeza kwamba, Watoto wa kike wengi wanapata ujauzito wakati wa kusbiria matokeo ya shule, au hata wengine kuolewa kabla ya kujiunga na kidato cha kwanza, wakati ni  kosa la jinai, kwa mujibu wa Sheria ya Elimu ya mwaka 1978 pamoja na kanuni zake.

Pia alipongeza uongozi wa shule hiyo kwa kuifanya kata ya Saranga kupaa kielimu kutokana na Shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma, katika mitihani ya Kitaifa, kimkoa na kiwilaya.

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya shule hiyo, Mwalimu Mkuu, Mariam Mbaya, alisema kwamba, shule imewekaza kwenye kumjenga mtoto kukua kinidhamu, kitaaluma na kujitambua.
“Mheshimiwa Mgeni rasmi, kama unavyowaona watoto hawa , wamejengwa kwenye misingi ya nidhamu, kujiamini, na kujitambua. Wanafunzi waliohitimu NABA wanajiamini, wanauwezo mkubwa wa kujieleza, na wanafaulu vizuri. Matokeo yetu kitaaluma ni mazuri sana. Na tunaendelea kujitahidi kufanya vizuri Zaidi” alisema Mwalimu Mkuu.

Shule ya awali na msingi NABA ipo katika manispaa ya Ubungo, kata ya Saranga.  

No comments:

Post a Comment