Thursday, September 15, 2022

CUF yatengeneza sera ya usawa wa Kijinsia

 

Na Mwandishi wetu, Unguja

Chama cha wananci (CUF) kimeanza mchakato wa kuandaa sera ya Jinsia ya Chama itakayotumika kurasimisha masuala ya kujinsia ndani ya chama kwa kipindi chote

Mchakato huu ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Baraza la Vyama vya siasa nchini lilolomwagiza Msajili wa Vyama vya Siasa kushirikiana na wadau ili kuviwezesha vyama vya siasa kuwa na sera ya Jinsia ili kuzingatia usawa wa kijinsia na kuongeza ushiriki wa wanawake, vijana, watu wenye ulemavu katika nafasi za uongozi na maamuzi ndani ya chama.

Mchakato huu unawezesha na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na shirika la Wanawake, Sheria katika Maendeleo Afrika (WilDAF), kwa kutoa wataalamu ambao wanajenga uwezo kwa watendaji wa CUF kuandaa rasimu ya sera hiyo.




Akizungumza wakati wa maandalizi ya rasimu hiyo, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Mbarouk Seif Salim, wakati wa kukaribisha wajumbe wa kikao kazi hicho kuanza kazi,  alisema kwamba, chama kimefurahi kwamba kimekuwa miongoni mwa vyama vya awali ambavyo vitatengeneza sera hiyo, na ana matumaini kuwa kazi hiyo itamalizika kwa wakati na kuleta tija ndani ya chama.

“sisi CUF ni chama cha siasa ambacho tumekuwa tukizingatia  usawa wa kijinsia, kwenye ushiriki wa wanawake tumejitahidi, bado hatujafikia 50:50 lakini tuna matumaini kuwa tutafanya vizuri sana baada ya sera hii kukamilika” alisema Naibu Katibu Mkuu.

Aidha Katibu wa Kikosi kazi, Ally Juma Khamis, alisema kwamba kwa niaba ya kikosi kazi hiyo, wameamua kujituma, kuhakikisha kazi hiyo ya kuandaa sera inakamilika kwa wakati na inawasilishwa kwenye vikao vya juu kwaajili ya kupata baraka na kuanza kutekelezwa.

“sisi tunashukuru Chama kwa kutuamini, kututeua tuwe sehemu ya maandalizi ya sera hii. Tumeaminiwa kuwawakilisha wenzetu, hatuta wangusha, tutahakikisha tunatoka na sera nzuri ya Kijinsia ambayo italeta mabadiliko makubwa ya usawa wa kijinsia ndani ya chama chetu” amesema Ally.


Upande wake, Mwezeshaji kutoka TGNP, Deogratius Temba, alisema kwamba yeye amefkia  CUF kwaajili ya kuwezesha watendaji wa chama kutengeneza sera hiyo, na kwamba mchakato huu unafanywa na chama chenyewe sio TGNP au WiLDAF.

“Sisi hapa ni wawezeshaji tu, kazi hii inafanywa na chama chenyewe, tunawawezesha kutambua masuala ya Kujinsia na namna ya kuyaweka ili yaeleweke, tunawawezesha pia kuwa na uwezo wa jicho la kijinsia , baadaye wanayaweka kwenye sera, hapa mimi nimekuwa nikijibu maswali yao zaidi, ninaamini hiki kikosi kazi kitamaliza kazi kwa wakati na kuanza utekelezaji wa sera hii”alisema Temba

Mchakato huu umehusisha kupitia nyaraka za chama zikiwemo Ilani, Katiba, Kanuni, sera, program na nyaraka nyingine za kiuendeshaji ili kuangali kwa namna zilivyozingatia usawa wa Kijinsia.

Washiriki wa kikosi kazi cha kaundaa sera ya Jinsia ya CUF wakiwa katika Picha ya pamoja
washiriki wa kikosi kazi cha kuandaa sera ya Jinsia ya CUF wakiwa katika Picha ya Pamoja
washiriki wa kikosi kazi cha kuandaa sera ya Jinsia ya CUF wakiwa katika Picha ya Pamoja

washiriki wa kikosi kazi cha kuandaa sera ya Jinsia ya CUF wakiwa katika Picha ya Pamoja

 

No comments:

Post a Comment