Saturday, September 10, 2022

MWANACHUO AJIKATA TUMBO BAADA YA KUMUUA MWANAFUNZI MWENZAKE DODOMA


Changamoto kubwa inayowasumbua vijana na jamii kwa ujumla ni kukosekana kwa uelewa juu ya umuhimu wa maisha ya mtu binafsi katika ulimwengu huu na wakati mwingine kupelekea watu wengine kuweka maisha yao rehani kwa watu wengine. 

matukio ya kujiua, kuua, kujeruhi, kuumiza, au kufanya vitendo vya Ukatili wa Kijinsia katika jamii vinashamiri sana na kwa kasi ya hali ya juu. Hii inatokana na kwamba, kuna ukosefu mkubwa wa maadili.  

Mwanafunzi wa Chuo cha St John, Winfrida Michael (24) amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu na mpenzi wake Julius Gervas (26) ambaye pia ni mwanafunzi wa chuo hicho sababu ikitajwa kuwa wivu wa mapenzi.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Martin Otieno amesema tukio hilo limetokea Septemba 7,2022 baada ya Julius kufanya mauaji hayo alijaribu kujiua kwa kujikata tumbo na sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Mkoa wa Dodoma.

Ofisa muuguzi wa hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Ester Ngoloki amesema walimpokea Julius akiwa na jeraha la kuc

No comments:

Post a Comment