CHAUMMA WAANDAA SERA YA USAWA WA JINSIA
Na Mwandishi Wetu,Dar
CHAMA cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), kimeanza mchakato wa
kuandaa sera ya Jinsia ya chama hicho kwaajili ya kuzingatia usawa wa Kijinsia
na kuongeza ushiriki wa wanawake, vijana
na watu wenye ulemavu katika nafasi za uongozi na maamuzi.
Azkiungumza wakati wa kikao kazi cha kuandaa rasimu ya Serya
ya Jinsia ya Chama hicho, Naibu Katibu
Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Tanzania bara Bw. Eugen Kabendera wakati wa Mafunzo Maalum ya namna ya
kuandaa Sera yalitotolewa na Shirika la Mtandao
wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na shirika la Wanawake na Sheria
Katika Maendeleo Afrika (WiLDAF) alisema kwamba, imefika mahali ambapo haiepukiki
kuwa na sera za usawa wa kijinsia kila nyanja za taifa letu.
Bw. Kabendera amesema kuwa Sera ya Jinsia ni muhimu katika
Taifa letu kwa kuwa inakwenda kulinda Haki za wanawake, vijana, wazee na watu
wenye ulemavu katika kufanya Siasa.
“ sisi kama CHAUMMA tunatamani kufanya siasa inayomshirikisha
mwanamke moja kwa moja. Ushiriki wa makundi yote, watu wenye ulemavu, vijana,
wazee, wajisikie sehemu ya siasa,wanufaike na siasa na mgawanyo wa nafasi za
uongozi uzingatie usawa” alisema.
Aidha ameongeza kuwa takwaimu zinaonyesha kuwa Wanawake
katika nchi hii ni wengi kuliko makundi yote lakini wamekuwa wakitumiwa vibaya
na kuwa kama njia ya kuwapitisha wanasiasa kupata uongozi, na CHAUMMA kimejipanga kuhakikisha kuwa sera ya jinsia itatoa
mweleko mzuri wa kuzingatia usawa wa Kijinsia katika nafasi za maamuzi na
uongozi.
Kwa upande wake Katibu wa jumuiya ya wanawake CHAUMMA Bi.
Marry Mpangala ameshukuru sana TGNP pamoja na WILDAF kwa kuweza kuwaletea mafunzo hayo na kusema
kuwa katika vyama vingi vya siasa ngazi za maamuzi zimekuwa zikishikiliwa na
wanaume na wanawake wamekuwa wakiachiwa nafasi ndogo ndogo.
Ameongeza kwa kuwataka wanawake waje kwa wingi ndani ya
CHAUMMA ili waweze kusogeza mbele Ajenda yao ya ‘Ubwabwa na Maharage’
kuhakikisha inawafikia wangonjwa Mahosptalini na Watoto Mashuleni, na kuongeza
kuwa wanawake wakati wa kujifungua wanapoteza damu nyingi hivyo wanahitaji
chakula cha kutosha ambacho ni Ubwabwa na Maharage.
Deogratius Temba, ambaye ni mwezeshaji wa mchakato huo
kwaniaba ya TGNP na WILDAF alisema kwamba, mchakato huo unafanywa na chama,
mashirika hayo yanawezesha kuweka sawa masuala ya Kijinsia ili sera hizo ziweze
kukamilika zikiwa zimeweka vizuri misingi ya usawa wa Kijinsia na ushiriki wa
wanawake katika nafasi za uongozi.
“Hii ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya viongozi wakuu
wa vyama vya siasa, baada ya kupatiwa mafunzo na TGNP na WILDAF na vikao kadhaa
vya mashauriano vilifanyika chini ya uratibu wa Ofisi ya msajili wa vyama vya
siasa, baadaye walikubaliana kwamba ili kufikia usawa wa Kijinsia ndani ya
vyama vya siasa na kuzuia vitendo vya Ukatili na udhalilishaji wa Kijinsia
ndani ya vyama ni muhimu kuwa na sera ya Jinsia” a;isema Temba
CHAUMMA kinakuwa miongoni mwa vyama vinane vya siasa nchini
Tanzania ambavyo vipo kwenye mchakato wa kuandaa sera ya Jinsia, kwaajili ya
kuweka mazingira salama kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kushiriki
kwenye nafasi za uongozi na maamuzi.
No comments:
Post a Comment