Saturday, June 8, 2024

Wananchi Kasulu, wataja maeneo hatarishi kwa Ukatili wa Kijinsia

 Wananchi Kasulu, wataja  maeneo hatarishi kwa Ukatili wa Kijinsia


Mwananchi wa Kata ya Kumsenga, akipanga mawe kama sehemu ya kubainisha sehemu hatarishi ambako kuna vitendo vya Ukatili wa Kijinsia katika Kata hiyo. Zoezi hili ni mbinu moja wapo ambayo hutumika wakati wa Utafiti shirikishi (Participatory Action Research).washiriki huwezeshwa kutumia mbinu za U-3 [Uibuaji, uchambuzi na Utatuzi]


Na Deogratius Koyanga, Kasulu

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Maataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), wamewawezesha wananchi kutoka kata mbili za Kumsenga na Murusi, katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu, kutambua, kuibua na kuainisha maeneo hatarishi ambapo vitendo vya Ukatili wa Kijinsia vinafanyika na kusababisha kutokea kwa mimba za utotoni.

Hayo yameibuliwa wkaati wa mrejesho wa zoezi la utafiti shirikishi (PAR) liliofanyika katika Halmashauri hiyo, kama sehemu ya utekelezaji wa mradi wa TGNP na UNFPA unaolenga kutokomeza vitendo vya Ukatili wa Kijinsia katika wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma.

Maeneo yaliyotajwa kuwa yanasababisha uwepo wa mimba za utotoni ni pamoja na; Masoko ya usiku ambayo husababisha ngono zembe bila kuangalia rika. Mfano,  Soko la CCM lililoko mtaa wa Omar, Soko Kuu lililoko mtaa wa Ikulu mjini na soko la kwa Shayo lililopo kata ya Murusi,  Masoko haya yanaanza saa kumi jioni na kumalizika kati ya saa nne hadi sita usiku.

“Wazazi kwenda kulima mashamba ya mbali na kuwaacha watoto peke yao majumbani, hali hii hupelekea watoto wakubwa kwenye familia hizi kuhemea kwa ajili ya wadogo zao, hivyo kulazimika kushiriki ngono ili kukidhi mahitaji ya familia zao” imeeleza sehemu ya risala ya wananchi iliyossomwa kwa Mkurugenzi wa Halmasahuri ya mji wa Kasulu.







No comments:

Post a Comment