Wednesday, June 5, 2024

Vitendo vya Ubakaji, ulawiti kero Kasulu

 Vitendo vya Ubakaji, ulawiti kero Kasulu


Washiriki wa Utafiti shirikishi wa Kiraghibish (participatory Action Research-PAR) kutoka kata ya Murusi, Kasulu Mjini, walijadiliana, kuchambua na kubaini sababu za kushamiri kwa vitendo vya Ubakaji katika eneo hilo. PAR ni shughuli inayotekelezwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na UNFPA katika Halmashauri hiyo.


 Na Deogratius  Koyanga, Kasulu

Wananchi wa kata ya Murusi, Halmashuri ya Mji wa Kasulu, mkoani Kigoma, wamesikitishwa na kushamiri kwa vitendo vya ubakaji na ulawiti kwa watoto.

Sababu zilizoibuliwa na wananchi hao, wakati wa zoezi la uraghibish  shirikishi (Participatory Action Research –PAR) ulioendeshwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu (UNFPA),  ni pamoja na Imani za kishirikina ambao hupelekea vitendo vya ulawiti kwa wanaume na ubakaji kwa wanawake na wasichana unaosababishwa na tamaa ya mali.

Aidha, sababu nyingine iliyoibuliwa ni unywaji wa pombe kupita kiasi kwa wazazi na kupelekea watoto kukulia vilabuni, na hivyo kukosa malezi stahiki. Pia unywaji pombe kupitiliza husababisha watu kubakwa au kubaka.

“hapa kwentu kuna tatizo la watu kudanyangwa na waganga wa kienyeji kuwa ili wapate utajiri wabake watoto wao. Mfano baba kubaka binti ili apate utajiri, na wanafamilia wengine kukaa kimya/kuyamaliza kifamilia” wamesema washiriki hao

Pia imeonekana kwamba, kuna vitendo vya Ubakaji kwa watu wanaoishi na ulemavu – mfano wagonjwa wa akili hadi kupewa mimba.





No comments:

Post a Comment