TGNP,UNFPA wajipanga kutokomeza Ukatili wa Kijinsia Kasulu
Na Deogratius Koyanga, Kasulu
Mtandao
wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirkiana na shirikal la Umoja wa matifa la
Idadi ya watu (UNFPA), wameiwezesha jamii inayoishi katika kata za Kumsenga na
Murusi katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu, kuanzisha Vituo vya taarifa na
Maarifa katika kata zao, ili kuendeleza harakati za kupambana na kutokomeza
vitendo vya Ukatili wa Kijinsia katika eneo hilo.
Wakiwasilisha
mrejesho wa utafiti uliofanywa na wananchi hao kw akuwezeshwa na TGNP na UNFPA,
wananchi hao mbele ya Menejimenti ya halmashauri ya Mji wa Kasulu, walisema
kwamba:
“…
baada ya utafiti huu, na kwa kuongozwa na TGNP, tumeunda kikundi cha kijamii
kinachoitwa Kituo cha Taarifa na Maarifa kwenye kila Kata, yaani Kituo cha
Taarifa na Maarifa Kumsenga na Kituo cha Taarifa na Maarifa Murusi. Vituo hivi
ni mahali ambapo wanajamii wote wa Kata zetu watapata fursa ya kupashana habari
na kupeana taarifa mbali mbali juu ya masuala yanayohusu jamii zetu ndani ya
mitaa na Kata, na taifa kwa ujumla. Tutashirikiana na viongozi wetu, na jamii
nzima kutatua changamoto zinazotukabili, ikiwa ni pamoja na kupambana na
ukatili wa kijinsia. Tunaamini kuwa jamii yenye usawa wa kijinsia ni jamii inayojitambua
na yenye maendeleo.”
Katika
risala hiyo, wameeleza kwamba kwenye mradi huo wa kupambana na ukatili wa
kijinsia, TGNP itaendelea kushirikiana na viongozi na wananchi wa Kata ya
Kumsenga na Murusi kupitia Vituo hivi vya Taarifa na Maarifa, pamoja na Ofisi
ya Mkurugenzi Halmashauri ya Kasulu Mji.
“..Ndugu
Mkurugenzi, sisi kama wazazi na jamii ambayo pia ni sehemu ya waliochangia
uwepo wa changamoto tulizozitaja hapo juu, tumeamua kubadilika na kuwa sehemu
ya kukemea na kutoa taarifa za wale wanaoendeleza changamoto hizo na hususani
ukatili wa kijinsia. Kama jamii tunatakiwa kuacha tabia ya kumaliza mambo hayo
kwa siri nyumbani. Tunaomba Polisi na watendaji wa serikali ngazi ya mitaa,
kata na wilaya watusaidie kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa na kupata hukumu
stahiki, nasi tutatoa ushirikiano wa kutosha katika kufanikisha hilo.
“….,
tunatoa shukurani za dhati kwa asasi hii ya TGNP kwa elimu hii; kwani
wametufumbua macho na sasa tuko tayari kushirikiana na viongozi wetu katika
kuhakikisha jamii yetu inashiriki vema katika kutatua changamoto mbalimbali
zinazotukabili. Aidha, tunaahidi kujenga jamii inayothamini utu wa kila mtu.”
Walisema washiriki hao ambao ni waanzilishi wa Vituo vya Taarifa na Maarifa
hivyo vipya.
Baada
ya kunzishwa kwa Vituo hivyo, TGNP sasa inakuwa na Vituo vya Taarifa na Maarifa
tisa (7) katika halmasahuri hivyi vikiwemo , Nyansha, Murufiti, Kigondo,
Muganza, Kigondo, Ruhita na Kumsenga.
No comments:
Post a Comment