Monday, June 10, 2024

TGNP na UNFPA wanzisha Vituo vya Taarifa na Maarifa Kasulu

 TGNP  na UNFPA wanzisha Vituo vya Taarifa na Maarifa Kasulu






Na Deogratius Koyanga,Kasulu

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana  na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu (UNFPA), wameunda Vituo vya taarifa na Maarifa kwenye Kata mbili za Kumsenga na Murusi, katika halmashairi ya Mji wa Kasulu

Kuunadwa kwa vituo  vya taarifa na Maarifa (KCs) katika Halmashauri hiyo kumefuatiwa na zoezi la utafiti shirikishi wa kiraghibish (PAR), ambao ulifanywa na TGNP kama sehemu ya Utekelezaaji unaotekelezwa na UNFPA kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji wa Kasulu na TGNP kwa lengo la kutokomeza Ukatili wa Kijinsia katika jamii ya Kasulu.

Kituo cha Taarifa na Maarifa kinachoundwa na TGNP ni sehemu ya kujenga na kuimarisha ujenzi wa nguu ya pamoja katika kusimamia harakati za kutokomeza vitnedo vya Ukatili wa Kijinsia. Katika jamii na kusimamia utekelezaji wa mipango kazi iliyoibuliwa wakati wa zoezi la uraghibish.

Tangu mwaka 2018, TGNP imekuwa ikifanya kazi katika halmasahguri hiyo na kuanzisha Vituo hivyo ambavyo vimeweza kufanya kazi kubwa ya uhamasishaji kwa wananchi kushiriki shughuli za maendeleo na kutokomeza vitendo vya Ukatili wa Kijinsia.

Vituo vya Taarifa na Maarifa vlivyoanzishwa mwishoni mwa wiki katika kata hizi mbili vinaenda kuunganisha nguvu na vingine ambavyo TGNP ilishaanzisha katika halmashauri hiyo, ambavyo ni Kata za Kigondo, Murufiti, Nyansha, Mganza. 

No comments:

Post a Comment