Friday, June 28, 2024

Jamii yaaswa kuteua ‘mangariba; wanaokubalika wenye maadili

 Jamii yaaswa kuteua ‘mangariba; wanaokubalika wenye maadili





NA Mwandishi wetu, Lindi

Jamii imetakiwa kuteua wataaamu wa kusimamia shughuli za jando na unyago ambao wanaheshimika katika jamii na kukubalika ili kuweka mazingira salama na kutoa elimu nzuri ya makuzi kwa jamii

Hayo yamesemwa na Afisa Mtendaji Kata ya Mchinga,Wiliam Mwang’onda, katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, wakati akitoa mrejesho kwa viongozi wa dini, mila, viongozi wa vikundi vya kijamii juu ya manafinikio yaliyopatikana kutokana na elimu iliyotolewa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwenye utekelezaji wa Mradi wa Uwezeshaji wanawake kushiriki kwenye uongozi na Maamuzi  na Haki ya uchumi unaofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya wanawake (UNwomen).

Akizungumza kwenye mdahalo wa jamii, uliowashirikisha wananchi kutoka makundi tofauti, kama sehemu ya mwendelezo wa midahalo ya makundi hayo, alisema kwamba, mradi huo umesaidiea kujenga uelwa kwa jamii juu ya kubadilisha mitazamo hasi, mila na desturi hasi, juu ya uwezo wa wananwake kuwa viongozi na pia kumiliki uchumi hasa ardhi na mazao yanayotokana na kilimo.

“tunaendelea kusisitiza na kutoa elimu ili jamii ibadilike. Tunaomba wanaotoa elimu ya jando na unyago wawe ni watu wanaokubalika na jamii, wenye maadili, na ambao wanataswira nzuri ili waweze kuwafundisha vijana wetu mambo mazuri ya makuzi yatakayowawezesha kuwa wazazi wazuri wa kesho kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla na watakaoweza kuzuia na kutokomeza vitendo vya Ukatili wa Kijinsia katika jamii” alisema Mwang’onda.

Kwa upande wake mchungaji wa kanisa la wa adiventista Wasabato, Mchinga, Yohana Mwihechi, alisema kwamba wao kama viongozi wa dini, ni washauri wa jamii kuhusu suala la maadili, na wataendeea kutoa elimu katika taasisi zao za dini ili kuwa na jamii inayojali usawa wa Kijinsia na kuheshimu haki na utu wa wengine.

“sisi ni sehemu ya wasimamizi wa madili mema na washauri wa jamii, tutaendelea kusaidiana na serikali katika kutoa elumu kwa jamii juu ya kuacha mila potofu, zinazochangia ukatili wa kijinsia na udhalilishaji, lakini zinazosababisha wanawake kutokumiliki rasilimali kama ardhi”alisema Mchungaji Yohane.

Awali akiwasilisha mafanikio ya mradi huo, mwezeshaji ngazi ya kata ambaye ni afisa Ugani Kata, Abduliazii Ngimbwa, Alisema kwamba baada ya kupatiwa mafunzo na TGNP kuhusu usawa wa Kijinsia, Bajeti yenye mtazamo wa Kijinsia na urasimishaji wa masuala ya KIjinsia kwenye jamii  kwa kushirikiana na maafisa wengine wa Halmashauri wamewezea kutoa elimu hiyo kwenye shule za msingi na sekondari, vikundi vya wanaume na wanawake na kufanikiwa kufikia Zaidi ya watu 3000, katika kata hiyo. 










No comments:

Post a Comment