Kwanini ni muhimu kuondoa kodi kwenye taulo za
kike?
Uchambuzi umefanywa na Deogratius Temba
Mnamo mwezi Julai 2018, Serikali ya Tanzania
ilipotoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa Taulo za Kike ilitoa ujumbe
wa wazi kwamba bidhaa hizi ni hitaji la Msingi la Haki za binadamu nani la
lazima kwa wasichana na wanawake.
Katika Hotuba ya Bajeti ya mwaka wa fedha
2018/2019, Waziri wa Fedha wakati huo, Dkt Philipo Mpango akasisitiza kwamba
wanawake na hasa wasichana wa shule wanaotoka katika familia masikini
wanahitaji kupata taulo za kike kwa bei nafuu na rafiki ili waweze
kujisitiri na kuhsiirki kwenye masomo au
shughuli za uzalishaji wakiwa salama.
Ilikuwa
ni hatua kubwa muhimu kuelekea usawa wa kijinsia, na kupunguza ‘Umasikini wa Hedhi’. Hatua hii ilisherehekewa
katika jukwaa la kitaifa na kimataifa. Tanzania ni kati ya nchi chache vinara
kutekeleza mpango huu, ikiiipiku nchi ya Australia (ambayo imeondoa kodi
Januari 2019), na nchi nyingine za ukanda na duniani.
 |
Picha hii imepatikana kwa hisani ya Mtandao |
Hatua hii ni muafaka kwa uchumi, na ingechangia
viwango wa ukuaji wa Taifa. Hata hivyo, Benki ya Dunia inakadiria kwamba, kwa
kila uwiano wa ongezeko la asilimia moja ya idadi ya wanawake wenye elimu ya
sekondari, pato la nchi la mwaka hukua
kwa asilimia
0.3.
Kwa nini Msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT) ni muhimu na Ubaki
Msamaha wa kodi ya
ongezeko la Kodi ya Thamani (VAT) kwenye taulo za kike ni muhimu kwa sababu kuu
mbili, ikihusianishwa na usawa wa kijinsia na pia unafuu wa Taulo za Kike.
Kuhusu usawa wa jinsia, wanawake na wasichana hawana hiari juu ya Hedhi.
Kuanzia umri wa miaka 13 – 55 wataingia kwenye Hedhi kwa kadiri ya wiki nzima,
kila mwezi.
Kulipa Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT) katika bidhaa za hedhi kunawafanya wanawake kulipa
kodi ya ziada wakilinganishwa na wanaume kiuhalisia kutokana na hali yao ya
kibaiolojia, kodi iko kwa watu wa jinsi moja.
Kuhusu unafuu, msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani una uwezo wa
kupunguza gharama ya taulo za kike kwa
asilimia 18, ambalo linaweza kuchangia bidhaa kupatikana kirahisi kwa wanawake
na wasichana nchini kote. Ni muhimu bidhaa hizi zikawa nafuu ili kuwasaidia
wanawake na wasichana kudhibiti Hedhi kwa usafi na utu.
Hedhi isichukuliwe kama njia ya kuongeza mapato, badala
yake upatikanaji wa bidhaa za hedhi uchukuliwe kama suala la haki za binadamu
na uswa wakijinsia, na iwe hivyo.
Serikali kuondoa VAT si tu inatambua bidhaa za hedhi kwamba ni bidhaa
‘muhimu’, lakini pia inawasaidia wanawake na wasichana kuzipata kwa unafuu na hivyo
kupunguza vikwazo wanavyokutana navyo kielimu na kiajira.
Athari ya Kuondolewa kwa VAT kwenye Soko
Uchunguzi wa awali
unaonyesha matokeo mbali mbali juu ya kuondolewa kwa VAT. Kuna tatizo kwenye msimamo wa bei
unosababishwa na mnyororo wa usambazaji, ambao humwacha muuzaji wa rejareja kuamua
bei ya mwisho. Changamoto kubwa ikiwa ni uzingativu wa bei kwenye bidhaa
zinazonunulika haraka kutokana na mfumo uliozoeleka. Hata hivyo kutokana na
kuondolewa na kwa VAT bidhaa za pedi zenye majina makubwa kama Always na HC
walithibitisha kushuka kwa bei kwa asilimia 20. Bidhaa nyingine pia zilionyesha
kupunguza bei kwa viwango tofauti, japo kwa kiasi kidogo.
Kwa kawaida wauzaji
wa rejareja ndio huchukua kiwango kikubwa cha faida kwenye mnyororo wa
usambazaji, na wao ndio wanabeba hatari na dhamana ya biashara na ndio wenye
ushawishi mkubwa juu ya bei ya mwisho (bei ya mlaji). Hatimaye, pamoja na
msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani, kunatakiwa pia kuwepo na kanuni na njia
madhubuti za ufuatiliaji kuhakikisha wauzaji wa rejareja wanazingatia
bei elekezi. Ushawishi wa bei ya rejareja ni jambo linalohitaji
mbinu, muda na uwekezaji na wadau kwa ajili ya kupeana taarifa.
Utafiti wa awali
uliofanywa Morogoro na Mbeya[1]
uliohusisha maduka 2,906 yanayouza taulo za kike (yakiwemo ya rejareja, ya
jumla, maduka ya dawa), inaonyesha kwamba bei ya bidhaa moja ikitofautiana kwa
asilimia 40 kutoka kwenye duka moja na jingine. Asilimia 52 inaonyesha pakiti
moja ya pedi ikiuzwa kwa Shilingi 2,000/=, Asilimia 13 zikiuzwa kwa shilingi
1500/= na asilimia 28 zikiuzwa kwa zaidi ya shilingi 2500/=.
Wahamasishaji wa Bei:
Pia, Utafiti huu unaonyesha
kwamba wakati mwingine bei inakuwa thabiti zaidi sehemu ambapo duka kuu linauza
bidhaa kwa bei ya chini kwa eneo husika. Hii inatoa fursa ya ushirikiano kati sekta ya umma na binafsi na
wahamasishaji wa bei katika kushusha bei katika maeneo ya jirani. Hasa, mara watumiaji wanapojua kuna maeneo
yanayoshindana wanayoweza kununua bidhaa, wana uwezo wa kuwa nguvu kubwa ya
kuleta ushindani katika soko, na kusababisha bei kushuka.
Utafiti wa awali wa soko unaonyesha kuwa
msamaha wa kodi ya VAT ulianza kupunguza bei. Hata hivyo, sera ya msamaha wa
kodi ya VAT imetekelezwa kwa muda mfupi chini ya mwaka mmoja, na huu sio muda
wa kutosha kuelewa na kupima athari zake.
Mapendekezo ya wadau ili kurudisha msamaha wa
kodi kwa pedi
Ni muhimu msamaha wa
VAT kubaki Tanzania. Hii ni hatua ya awali muafaka ya upunguzaji wa gharama za
bidhaa za Hedhi. Ikiwa wanawake na wasichana watakuwa na uwezo wa kumudu
gharama za pedi, haya yatakuwa ni mapinduzi makubwa yatakayowawezesha kutumia
muda wao kwenye kazi za uzalishaji na kielimu, na pia kuboresha afya zao.
Kwa ujumla wake hayo yote yatachangia kwenye
ukuaji wa uchumi wa Taifa, kupunguza mzigo kwenye sekta ya afya, na pia
kuhakikisha wanawake na wasichana wanatoa mchango kwenye sera ya viwanda na
Dira ya maendele ya Taifa ya 2025.
Ili Msamaha wa kodi
ya VAT uweze kufanyakazi kama ilivyotarajiwa ni vyema serikali na sekta binafsi
kufanyakazi kwa karibu, kuhakisha utekelezwaji wa ushushaji wa bei. Pia usimamizi
kwenye serikali za mitaa kunaweza kuleta tofauti katika kuongeza uelewa na
utekelezaji. Wauzaji wa rejareja waelimishwe kwamba bidhaa za Hedhi ni bidhaa
muhimu kwa akina mama na si anasa. Pia,
Serikali na Sekta binafsi itumie fursa ya kuona matokeo chanya ya kufanyakazi
pamoja ili kuleta matokeo mapana, vile vile watumie washawishi kwenye jamii.
Kuhamasisha watumiaji
na kuwaeleza juu ya msamaha wa VAT na kuwapa bei elekezi, itachagiza bidhaa
kushuka bei hasa kwa wauzaji wa rejereje na itaongeza msukumo kwa wauzaji wa
rejareja kushusha bei ya bidhaa yenyewe. Kampeni za kitaifa zinaweza kusaidia
jitihada hii, ikiambata na kutengeza hitaji kubwa katika soko.
Pamoja na kwamba
Serikali imependekeza punguzo la asilimia 5 ya kodi ya Makampuni. Hii ina hatari
ya kutoweza kubadilisha bei za pedi ikiwa hakuna kanuni na ufuatiliaji wa bei,
wanfanya biashara wa reja reja wanaweza kuendelea kujiongezea faida. Mwaka ujao
wa fedha 2023/2024 uwe ni fursa nyingine ya kuendelea kuwa na msamaha wa kodi
ya VAT kwa Taulo za Kike, na kufuatilia athari yake kwa karibu ili vikwazo
viweze kutatuliwa. Tanzania inatakiwa
kuendelea kuwa kinara wa dunia kwenye jambo hili ili wengine wafuate na
wajifunze kwetu. Uchambuzi umefanywa na Deogratius
Temba-0784686575