TGNP yapongeza Kikosi kazi cha Rais Samia
Na
Mwandishi wetu, Dar
Mtandao
wa Jinsia Tanzania (TGNP), imepongeza Kikosi kazi kilichoundwa na Rais Samia
Suluhu Hassan kwa mapendekezo yaliyotolewa, kwa lengo la kuboresha demokrasia ya
vyama vingi nchini.
Bi. Lilian Liundi, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP
Taarifa
iliyitolewa Jijini Dar es salaam, na Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Bi. Lilian
Liundi imeeleza kwamba:- “…Kikosi kazi
hiki kupitia Mwenyekiti wake, Prof. Rwekaza Mukandala, kimeweza kukabidhi
taarifa yake kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan yenye mapendekezo 18, ikiwemo mapendekezo
yenye lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake na makundi yaliyo pembezoni katika
uongozi na siasa. Miongoni mwa mapendekezo hayo ni pamoja na
I.
Pendekezo la. 5:
Katika uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi walau wajumbe wawili wawe
wanawake, na sifa za kuwa Mwenyekiti, Makamu au Mjumbe ziainishwe.
II.
Pendekezo la 11:
Sharti la uwepo wa Sera ya Jinsia kwenye Chama cha Siasa na ujumuishi wa
makundi maalumu. Utararibu wa Viti maalumu uendelee ila sheria ziboreshwe na kuweka
ukomo wa miaka 10 na pia, ushiriki wa wanawake katika vyombo vya maamuzi
usipungue asilimia 40.
III.
Pendekezo na. 12:
sheria zinazo kwamisha ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye siasa ziangaliwe
upya
IV.
Pendekezo na. 13:
juhudi za ushirikishwaji wa vijana kwenye siasa ziongezwe
Ni
matumaini yetu kuwa mapendekezo haya yatachukuliwa na kutekelezwa kwa haraka
ili kuweza kufikia malengo ya kuwa na demokrasia ya vyama vingi jumuishi na
itakayoleta tija katika maendeleo ya taifa letu.
Kipekee,
tunatoa pongezi pia kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Mwenyekiti wa
Baraza la Vyama vya Siasa kwa kuwa sehemu ya mchakato huu kwenye kikosi kazi na
kuweza kubeba na kuhakikisha ajenda ya masuala ya jinsia yanajitokeza katika
mapendekezo hayo.
Ikumbukwe
kuwa, mnamo mwezi Februari mwaka huu, chini ya mradi wa kuongeza ushiriki wa
wanawake katika uongozi unaotekelezwa na TGNP kwa kushirikiana na WiLDAF,
tuliweza kufanya kikao cha mashuriano na Baraza la Vyama vya Siasa, Ofisi ya
Msajili wa Vyama vya Siasa na Kikosi Kazi hiki cha Kuratibu maoni ya wadau kwa
lengo la kuangalia mapengo ya kijinsia ndani ya vyama vya siasa na kukubaliana
namna bora ya kuziba mapengo hayo ili kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi
za uongozi na maamuzi ndani na nje ya vyama vya siasa. Miongoni mwa mapendekezo yaliyotoka katika
kikao chicho cha mashauriano ni pamoja na uwepo wa Sera ya Jinsia katika vyama
vya siasa.
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, akipokea taarifa ya mapendekezo ya kikosi kazi kutoka kwa Mwenyekiti wake, Prof. Rwekaza Mkandala, Ikulu Jijini Dar es salaam
TGNP
tunaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na Baraza la Vyama vya Siasa na Ofisi ya
Msajili katika kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo hayo yaliyotolewa na
kikosi kazi na kuhakikisha kuwa kwa pamoja tunaweka misingi imara ya kuongeza
ushiriki wa wanawake katika uongozi wa siasa na ngazi za maamuzi. Tunatambua
mchango wa Kikosi Kazi, Baraza la vyama vya Siasa na Ofisi ya Msajili wa Vyama
vya Siasa katika kuleta mabadiliko na usawa wa kijinsia nchini.
Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan akiwa na wajumbe wa Kikosi kazi Ikulu Dar es saalam
No comments:
Post a Comment