Monday, October 17, 2022

Mambo muhimu kwa vyombo vya habari kukabiliana na Ukatili

 

Mambo muhimu kwa vyombo vya habari kukabiliana na Ukatili

Na Mwandishi Wetu.

SERA ya Jinsia ya vyomvo vya habari ya mwaka 2019, inavitaka vyombo vyote vya habari kuzingatia yafuatayo ili kuepuka kuwa sababu au chanzo cha ukatili wa kijinsia.  Vyombo vya habari vitaepuka kuunga mkono chuki au kushadidia ukatili wa kijinsia. Vitapaswa kuepuka mambo yafuatayo:

 Kutangaza au kuchapisha kwa kinagaubaga habari za ubakaji au ukatili wa kingono kwa namna ambayo itafanya waathirika watambulike;

Kushadidia picha chafu na za ukatili dhidi ya wanawake na watoto;

Kuwadunisha wanawake kwa kuwabainisha kama viumbe dhalili wanaostahili kufanyiwa ukatili, labda tu pale ambapo ukatili ni sehemu ya habari inayosimuliwa;

Kuwadunisha ama kuwatumia vibaya wanawake kwa kuwaonyesha kama viumbe dhalili wasio na uwezo wa kufanya lolote mbele ya ukatili na unyanyasaji;

Kuwadunisha au kuwatumia vibaya wanawake na kuhujumu nafasi chanya waliyo nayo, na umuhimu wao katika jamii;

Kushadidia unyanyasaji wa mawazo[1]mgando juu ya jinsia, na

Kuchapisha habari ambazo zinaweza kuibua vurugu na chuki kutokana na uwasilishaji mbaya wa masuala ya jinsia au kutukuza ukatili dhidi ya wanawake

No comments:

Post a Comment