Monday, February 3, 2025

Waves of Change: Kidimbwi Beach Unites for a Greener, Safer Future

 Waves of Change: Kidimbwi Beach Unites for a Greener, Safer Future


By Deogratius Temba

Global Impact Transformation (GIT), in collaboration with the Local Government of Mbezi Beach and various environmental stakeholders, spearheaded a highly successful clean-up at Kidimbwi Beach.

The initiative aimed to restore the coastline’s natural beauty and underscored the urgent need for environmental stewardship and social responsibility. Through addressing waste pollution, promoting climate action under Sustainable Development Goal (SDG) 13, and fostering community unity, the event highlighted the intersection of environmental sustainability and public safety, including gender-based violence (GBV) concerns, aligning with SDG 5: Gender Equality.

The clean-up brought together a diverse group of participants, including local government leaders, students, environmental advocates, and GIT Champions. Ms. Sylvia Mkomwa, GIT’s Communication Specialist and General Manager at Calabar Group of Companies, officially inaugurated the event, emphasising the power of collective action.

“When communities unite to protect their environment, we create ripples of change that extend beyond conservation. A cleaner, safer beach is not just about aesthetics, it’s about ensuring that everyone, especially women and children, can enjoy public spaces free from threats and vulnerabilities,” she stated.

Volunteers engaged in two primary activities waste removal and tree planting. They collected plastic waste, discarded bottles, and other hazardous materials that endanger marine life and beachgoers. By eliminating these pollutants, the initiative improved safety, reduced health risks and rejuvenated the coastal ecosystem.

In addition, trees were planted along the beachfront to prevent coastal erosion and enhance biodiversity. These efforts contribute to long-term environmental sustainability, ensuring that future generations inherit a healthier planet.

Beyond its ecological benefits, the clean-up also served as a platform to address social challenges such as GBV and gender inequality, reinforcing SDG 5: Gender Equality. Polluted and neglected public spaces can become hotspots for insecurity, disproportionately affecting women and girls. Unsafe environments discourage free movement and limit access to recreational and economic opportunities.

Moreover, women’s involvement in sustainability initiatives is a crucial step toward inclusive leadership and social transformation. The active participation of female leaders, volunteers, and youth in the Kidimbwi Beach Clean-Up demonstrated that environmental advocacy can also serve as a tool for social empowerment and gender equality.

Martha Ng'hambi, the Executive Director of GIT, also highlighted the organization's commitment to making the environment safe and clean through collaboration with local government. "At GIT, we believe that protecting the environment goes hand in hand with ensuring the safety of the community, especially for women and girls who frequently use public spaces like beaches. Through our partnerships, we aim to create secure, well-maintained environments where everyone can thrive without fear," she stated.

The success of the Kidimbwi Beach Clean-Up serves as a reminder that maintaining clean and safe coastal areas requires sustained effort. Regular clean-up campaigns, environmental education programs, and stronger collaborations between stakeholders are key to preserving these achievements.

As the event concluded, many participants expressed their commitment to making environmental conservation a lifestyle, not just a one-time effort. “A clean environment fosters not only ecological health but also human dignity and security,” one volunteer remarked.

Intertwining environmental action with social advocacy, the Kidimbwi Beach Clean-Up exemplifies how local initiatives can drive meaningful, lasting change one wave at a time

















 

Monday, January 27, 2025

“upatikanaji wa huduma za hedhi salama, ulivyo tejesha tabasamu kwa wasichana shuleni ”


Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Zirai, Wilayani Muheza mkoani Tanga, wakiwa na Mwandishi wa Makala hii wakati alipotembelea shuleni hapo.

Na deogratius temba, Muheza

Mwongozo wa serikali juu ya Maji, Afya na Usafi wa mazingira wa mwaka 2016, unatoa maelekezo kwamba wadau  katika ngazi mbalimbali watahusika kusimamia utekelezaji wake ikiwepo kuhakikisha kuwa ujenzi wa miundombinu ya hedhi salama katika shule unakuwa na tija. Serikali kupitia wmongozo huo ulioandaliwa na Wizara ya elimu, sayansi na Mafunzo ya Ufundi, inazotaka kila Halmashauri kusimamia utekelezaji wa mwongozo huo ikiwa ni pamoja na kutenga bajeti kwa kila mwaka wa fedha kwenye mapato yake ya ndani ili kutatua changamoto zinazotokana na kukosekana kwa huduma nzuri kwenye eneo la Maji, afya na usafi wa mazingira (SWASH)  na kusababisha kiwago cha elimu kushuka.

Kama sehemu ya utekelezaji wa mwongozo huu wa serikali, Mtandao wa Jinsia (TGNP), kwa kushirikiana na Shirika la ONGAWA na  Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, wanatekeleza mradi wa Maji, afya na usafi wa mazingira (WASH) katika ngazi ya kaya na shuleni, ambapo suala la Hedhi salama shuleni linapewa msukumo wa kipekee ili kuwezesha wasichana kushiriki kikamilifu masomo shuleni wanapokuwa kwenye hedhi.  Utafiti wa awali kuhusu hali ya SWASH uliofaywa na serikali mwaka (2009) katika shule za msingi na sekondari iliyofanyika katika wilaya 16 Tanzania umeoneshasha kwamba hali ya Maji, Usafi wa mazingira katika shule ilikuwa chini. Ni asilimia 11 ya shule zilizofayiwa utafiti ndizo zilikuwa zimefikia hitaji la kisera la uwiano wa matundu ya vyoo wa Tundu moja kwa wasichana 20, na tundu moja kwa wavulana 25. Zaidi ya asilimia 20 ya shule zilikuwa na uwiano wa wanafunzi 100 na zaidi kwa tundu moja la choo. Wakati utafiti ulionesha kuwa asilimia 6 ya shule zilikuwa hazina kabisa matundu ya vyoo.

 

Picha halisi inaonesha kuwa utafiti huu wa Maji, Afya na usafi wa mazingira shuleni (SWASH), shule nyingi hazina miundombinu ya kutosha ya usambazaji wa maji, miundombinu hafifu ya usafi wa mazingira, hakuna kabisa mfumo wa kunawa mikono, baadhi ya vifaa vya usafi  ni vibovu au vimevunjwa.

Vifaa vya Maji, afya na usafi mazingira shuleni (SWASH) kama matundu ya vyoo, kwa shule nyingi hayalengi mahitaji ya wasichana wanapokuwa kwenye hedhi, watoto wadogo na wanafunzi wenye ulemavu, maeneo mengi yana mahudhurio hafifu kwa wasichana wanapokuwa kwenye hedhi kutokana na kukosekana kwa vifaa vya hedhi salama na usiri wa kujisitiri wakiwa kwenye hedhi.

Hivi karibuni, wasichana wa shule ya sekondari ya Zirai iliyoko katika Tarafa ya Amani -wilaya ya Muheza, walitoa sauti zao kushukuru wadau kwa kusaidia upatikanaji wa chumba maalum cha kujisitiri wanapokuwa kwenye hedhi, upatikanaji wa pedi za bure shuleni, maji safi na salama chooni, elimu na malezi bora ya makuzi yanayotolewa na waalimu wa kike shuleni hapo. Wanafunzi wamesema kwamba, sasa wanawea kusoma bila tatizo kutokana na kupata huduma za hedhi salama  shuleni na wengi waliokuwa hawafiki shuleni wakati wa hedhi.

Kwa upande wake Afisa Elimu Kata ya Zirai, Mwalimu Mohamed Mmole, anazungumzia mafanikio ambayo shule yake ya kata ya Zirai imeyapata kutokana na uwepo wa vyumba maalum vya kujisitiri kwa wasichana wakati wa hedhi pamoja na upatikanaji wa pedi shuleni. Anasema kwamba uongozi wa shule ulikubaliana kuwa suala la hedhi salama lipewe kipaumbele.  Pamoja na changamoto ya ukosefu wa rasilimali fedha za kununua pedi na vifaa vingine, walikubaliana kutumia fedha kidogo za ruzuku ya elimu kwa wanafunzi (capitation) inayotolewa kwaajili ya afya shuleni na kununua vifaa hivyo.

“……. inawezekana kabisa kusimamia vizuri utekelezaji wa mwongozo huu wa serikali wa Afya, Maji na usafi wa mazingira wa mwaka 2016, wadau wametujengea matundu ya vyoo na chumba maalum cha kujisitiri, sisi hapa shuleni tumeamua kuunga mkono juhudi hizi za wadau kwa kuhakikisha hizi pedi hazikosekani, dawa za kutuliza maumivu kwa kwaajili ya wasichana nazo hazikosekani” anasema Mwalimu Mmole.

Mwalimu Mmole anasema kwamba, pamoja na changamoto ya miundombinu ya usafiri katika kata, ukosefu wa maduka karibu na wananchi, uwepo wa huduma muhimu za kiafya kwa wanafunzi kunaongeza ushiriki wa wanafunzi hasa wasichana kwenye masomo, ikiwepo ongezeko la mahudhurio darasani.

Mwalimu mlezi wa wasichana shule ya sekondari Zirai,  Rehema Matuga, anaeleza:  “ Sisi kama waalimu tunashukuru sana, tunapoona wasichana wana utulivu hapa shuleni, awali kabla ya miradi hii ya  hedhi salama haijaanzishwa hapa kwetu, suala la hedhi kwa wasichana hatukulipa kipaumbele, watoto wa kike walikuwa wakijiamulia kutokufika shuleni, lakini kwa sasa wanafika shuleni hata wakiwa kwenye hedhi na wanajua tutawasaidia vifaa na mazingira ya shule ni salama. Tunaishukuru sana TGNP na ONGAWA, shule yetu kwa sasa imekuwa mfano wa kuigwa”.

Laya Christopher, mwanafunzi wa kidato cha nne, shule ya sekondari Zirai anaeleza kwamba tangu huduma za hedhi salama zimeboreshwa shuleni hapo na kuwepo kw a chumba maalum cha kujisitiri, kuna mabadiliko makubwa ya ushiriki wa wasichana darasani.

“Utaona tu kila msichana anauhuru, anatabasamu muda wote, Kwa kweli sisi wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari Zirai, tunashukuru sana, kwa sasa hapa shuleni tunaona na mahali salama kwetu, baadhi yetu hata hizo pedi huko nyumbani zilikuwa hazipo, lakini sasa hivi zipo shuleni, ukiwa kwenye hedhi, unaona ni bora kuwepo shuleni hautachafuka, utakuwa salama na hautapata aibu, ukienda nyumbani utajua la kufanya, lakini jambo la msingi hapa shuleni umeshashiriki vizuri vipindi vya masomo na kujisitiri vizuri”. Anaeleza Laya

 

Kwa upande wake Amina Ayubu wa Kidato cha kwanza, anaeleza mtazamo wake kwamba yeye ametokea shule ya msingi mwaka jana 2020, ambako hakuwahi kuona au kusikia suala la hedhi likipewa kipaumbele au kujadiliwa kama ilivyo kwa shule hiyo ya Zirai.

“nilipofika hapa kuanza kidato cha kwanza, nimefurahi sana, nilijisikia vizuri kuona waalimu wanazungumzia suala la hedhi na kuteuelekeza nini cha kufanya tukiingia kwenye hedhi, tumesaidiwa ushauri na waalimu na pedi tunapatiwa hapa shuleni, kwa kweli sina hofu tena juu ya hedhi, ninajua nikiwa hapa Zirai nitasoma vizuri na nitafaulu..”alisema Amina.

Kwa upande wake Afisa Programu kutoka ONGAWA, Leonia Andrew anasema kwamba lengo la ONGAWA kuboresha mazingira ya utoaji elimu kwa watoto wa kike ni kuongeza kiwango cha elimu kwa wasichana na kuwafanya wahitimue elimu yao ya sekondari wakiwa kama wavulana.

“…Tunategemea viongozi wetu ambao wamefanyiwa mafunzo ya umuhimu wa kuboresha miundombinu ya hedhi  salama, maji, afya na usafi wa mazingira watasaidia kuhakikisha wanalipa kipaumbele, pia kwenye bajeti zetu tulipe kipaumbele. Sisi wadau tunachoomba ni kwamba suala hili liwe na utashi wa wananchi wa hapa na serikali yao, hata kama miradi inafikia ukomo, haya mambo yote yanatakiwa kuendelea hapa kwa manufaa ya watu wa Zirai” alisema Leonia.

Kaimu afisa Mtendaji kata ya Zirai, Florence Mosha anasema kwamba, kila kijiji kinatakiwa kuchukua hatua za dhati za kutekeleza mpango kazi na vipaumbele tulivyokubaliana hapa, ili tuweze kuwa na kata ambayo inazingatia usawa wa kijinsia. “……Kila kitongoji mkafanye kikao na kurejesha kwa wananchi masuala haya ya bajeti yenye mrengo wa kijinsia na kuweka mbele masuala ya hedhi salama kwa wasichana  katika shule zetu”.alisema Mosha

Shule ya secondary ya Zirai ina wasichana zaidi ya 150, ambao kwa sasa wanatumia pedi boxi 10 kwa mwezi. Pedi hizo zimekuwa zikichangiwa na wadau mbalimbali, shule kununua kutoka kwenye bajeti yake ya capitation na Kituo cha Taarifa na Maarifa Zirai ambao wamekuwa wakichangishana na kutafuta wadau mbalimbali.

Wakati wa mafunzo ya uandaaji wa bajeti kwa mrengo wa kijinsia kwa kuzingatia uboreshaji wa miundombinu ya hedhi salama kwa viongozi wa kata ya zirai yaliyofanywa na TGNP na ONGAWA, wenyeviti wa vijiji  vitatu vinavyounda kata hiyo, Kwalumbizi, Zirai na Kizerui, walisema kwamba kila kijiji kimeweka kipaumbele cha kuhakikisha shule za msingi zina miundombinu ya hedhi salama ikiwepo vyumba maalum vya kujisitiri pindi wakiwa kwenye hedhi na kutenga bajeti ya kununua pedi kwaajili ya wanafunzo shuleni.

Pamoja na vyumba maalum, kipaumbele kinawekwa pia kwenye kuhakikisha kila shule ya msingi ina sehemu ya kuchomea taka mbichi na kavu (incinerator) ili kuhakikisha pedi zilizotumika shuleni zinateketezwa na wanafunzo mara baada ya kutumika.

Mwisho 

Thursday, October 17, 2024

TGNP yaendesha utafiti raghibish kata ya Mgagao Mwanga


 

TGNP yaendesha utafiti raghibish kata ya  Mgagao Mwanga

  • ·       Wanachi Mgagao Mwanga wana na mapendekezo

Na Deogratius Koyanga

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), umewawezesha wananchi kutoka kata ya Mgagao, Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, Mkoani Kilimanajro kuendesha zoezi la utafiti uraghibish ili kutokomeza vitendo vya Ukatili wa Kijinsia na kukuza usawa wa Kijinsia.

 

Zoezi hilo ni sehemu ya mradi wa  Kuvunja vikwazo: kuondoa na kutokomeza Ukatili wa Kijinsia na Kukuza usawa wa Kijinsia  unaotekelezwa na TGNP katika halmashauri hiyo. Ambapo jamii imejengewa uwezo namna ya kuibua, kuchambua na kuweka mikakati ya utatuzi wa changamoto zinazowazunguka kwa kushirikiana na viongozi katika ngazi mbalimbali, sambamba na kuundwa kwa Kituo cha Taarifa na Maarifa katika kata hiyo.

 

Miongoni mwa changamoto za ukatili wa kijinsia zilizoibuliwa na kuwasilishwa mbele ya Mkururgnzi Mtendaji wa Wilaya ya Mwanga, Bi. Zuhura Msangi, na wakuu wa Idara na Vitengo ni pamoja na Suala la kushamiri kwa vitendo vya Ukatili wa Kijinsia kama vile Ubakaji kwa wanawake hasa wasichana, mimba za utotoni, ukeketaji wa wasichana na kuongezeka kwa uporaji wa mali hasa mifugo.

Katika mapendekzo yao, washiriki wa uraghibish huo, walipendekza kwamba;

Halmashauri iweke sheria kali za vijiji na wasimamizi wa sheria (Polisi na mahakama) na vyombo vingine zifanye kazi kwa uadilifu ili sheria itekelezeke. Halmashauri isimamie mchakato wa uandaaji wa bajeti uwe shirikishi kuanzia ngazi za kijiji ili tuwe na bajeti yenye mrengo wa Kijinsia itakayogusa mahitaji ya kila kundi.

Kuuhuisha kamati za Ulinazi wa Mama na Mtoto (MTAKUWWA) katika kata na vijiji vyote, zitambue majukumu yake na mfumo wa uwajibikaji yaani ziwe na taarifa zake za utekelezaji.

Mwongozo wa serikali (Feb. 2022) wa kuwarudisha wanafunzi walioacha masomo kwa sababu mbalimbali uanze kutumika ndani ya Kata. Mratibu Elimu Kata (MEK) aanze kuwabaini wasichana walioko mitaani na kuwarudisha shuleni kwa mujibu wa mwongozo.

Halmashauri isaidie usimamizi  na utekelezaji wa sheria ndogo ambazo zitathibiti watoto wa shule kuzurura hovyo siku ya Ijumaa mnadani na katika  magenge na kwenye vibanda vya kuoneshea Video.

Sheria kali zichukuliwe dhidi ya kutokomeza Mimba na ndoa za utotoni. Maafisa Ustawi wa jamii na Maendeleo ya jamii washirikiane na dawati la Jinsia na Mtoto-Polisi, kuharakisha kesi za ubakaji na wanaobainika wahukumiwe kwa mujibu wa sheri zetu.

Halmashauri isimamie watendaji wa Vijiji kufanya mikutano ya kisheria ya vijiji sambamba na mikutano maalum ya kuibua na klujadili vipaumbele vya Bajeti au miradi ya maendeleo (Mchakato wa uibuaji wa fursa na vikwazo katika maendeleo-[O&OD]. Ili kuweka kipaumbele masuala muhimu kama haya ya maji, mabweni nk.

Mradi wa umeme wa REA wa Kijiji cha Pangaro, uweke kipaumbele kwenye shule za msingi, zahanati  ili kuboresha huduma na kuwavutia watumishi kufanya kazi katika maeneo hayo

Kuendelea kushirikiana kati ya jamii na serikali kutoa elimu na kuzuia vitendo vya Ukeketaji katika jamii ya Mgagao hasa vitongoji vinavyotajwa kuwa na mila hizo.

Kwa upande wa menejimenti ya Halmashauri, waliahidi kusimamia utekelezaji wa mapendekezo haya, ikiwa ni pamoja na kuwezesha utekelezaji wake katika ngazi za chini sambamba na ujenzi wa Bweni kubwa la kisasa ambalo litaanza kujengwa hivi karibuni katika shule ya sekondari ya Mgagao.

Kuhusu suala la maji, mwakilishi wa wakala wa Usimamizi na usambazaji wa Maji Vijijini (RUWASA) alisema kwamba maji ya mradi wa Mwanga,Same Hedaru ayanayokatiza katika kata hiyo ataanza kutumika katika kijiji cha Mgagao na vitongoji vyake sambamba na shule ya sekondari Mgagao hivi karibuni. 















































Friday, September 20, 2024

WaterAid, TGNP na TAWASANET wajenga uwezo kwa wanawake Hanang’

 WaterAid, TGNP na TAWASANET wajenga uwezo kwa wanawake Hanang’


Picha ya pamoja ya washiriki wa mafunzo ya wanawake viongozi wa Halmashauri za vijiji na kamati mbalimbali wilayani Hanang' Mkoa wa Manyara


Na Deogratius Koyanga, Manyara

Taasisi ya WaterAid Tanzania,  Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), na Mtandao wa Asasi za Kiraia zinazoshughulikia Maji, na Usafi wa Mazingira Tanzania (TAWASANET), wamefanya mafunzo ya kujenga uwezo kwa wanawake viongozi kutoka vijiji nane (8) katika Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Mkoani Manyara.

Mafunzo hayo yanalenga kujenga uwezo kwa viongozi wanawake wanaohudumu kwenye Kamati za zahanati na Vituo vya afya, shule za msingi, Bodi za Sekondari na kamati za Huduma za jamii kwenye Halmashauri za vijiji ili waweze kuweka kipaumbele cha upatikanaji wa rasilimali ili kutatua changamoto za maji na Usafi wa mazingira (WASH) katika maeneo yao.

WaterAid, TGNP na TAWASANET  wanatekeleza kampeni ya Afya ya Mwanamke Sasa ambayo inalenga kujenga uwezo kwa wanawake na wanaume ili kuondoa changamoto za Kijinsia kwa kuzipa kipaumbele wakati wa mipango na bajeti sambamba na kuondoa changamoto za kijinsia ambazo zina wakabili zaidi wanawake.

Akiungungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkuu wa Ushawishi,  na Uchechemuzi wa sera kutoka WaterAid, Christina Mhando, alisema kwamba suala la ukosefu wa maji ni suala la wanawake, na ni suala la kijinsia, kwahiyo wanawake wanapaswa kulipa kipaumbele katika majadiliano, au maamuzi ya kupanga vipaumbele vya bajeti. “ …. Hata yanapoibuka magonjwa, waathirika wakubwa ni wanawake ndio maana tunashirikiana na wenzetu hawa kujenga uelewa wa jamii  jinsi ambavyo masuala ya maji, afya na usafi wa mazingira unavyoweza kuathiri wanawake, watoto wa kike na wazee  sambamba kurasimisha masuala ya kijinsia katika sera, bajeti na mipango yote ya serikali za Mitaa” alisema Mhando.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hanang, Theresia Irafy, wakati wa kufungua mafunzo hayo alisema kwamba, mafunzo hayo ni muhimu kwa wakati huu ukizingatia kwamba wanawake ndio wahitaji  na watumiaji wakubwa wa huduma za maji na endapo watapata uelewa na kusimamia vizuri rasilimali za umma sambamba na miradi iliyojengwa italeta tija na kuwezesha kumtua mwanamke ndoo kichwani.

“Ninashukuru wadau hawa kwa kuja Hanang, tunahitaji sana wadau wanaofanya kazi ya kujenga uelewa kwa jamii na kubadilisha mitazamo hasi kuhusu masuala ya kijinsia, mtawezesha kubadilisha mitazamo ya jamii, lakini pia wanawake wanatakiwa kuwa viongozi wazuri wa kusimamia miradi hii sambamba na kuibua  na kuweka vipaumbele vya bajeti vyenye mtazamo wa kijinsia” alisema

Mafunzo hayo pia, yamefungwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Bi. Rose Kamili ambaye alisema kwamba  suala la maji na usafi wa mazingira ni suala la kijinsia na linatakiwa kuwekewa mkazo kwa wanawake kulielewa na kulisimamia wenyewe kwasababu  ndio kundi linaloathirika zaidi endapo huduma za maji na usafi wa mazingira zitakosekana.

“Sisi Halmashauri, tunaendelea kupambana kuhakikisha tunatatua changamoto za ukosefu wa maji kwa baadhi ya maeneo, lakini tuendelee kuwashukuru wadau wetu WaterAid kwa kuwezesha upatikanaji wa maji safi na salama kwa baadhi ya vijiji hasa kwenye taasisi kama zahanati ambako wanawake wanapata huduma zaidi. WaterAid mmekuwa msaada mkubwa kwa wanawake wa Hanang, tunawashukuru sana…” alisema Kamili.

Mafunzo hayo yamewahusisha wanawake kutoka vijiji nane ambavyo ni Gidamula, Gawidu, Muungano, Dajameda, Laghanga,  Wareta, Getak na Bashang, ambapo  washiriki wamekubaliana kuhakikisha wanahamasisha wanawake kujitokeza kugombea uongozi katika serikali za Mitaa mwaka huu 2024 ili waweze kuwa kwenye nafasi za maamuzi hasa kuibua miradi ya maendeleo itakayotatua changamoto za Maji, afya na usafi wa mazingira (WASH) katika jamii.












Picha ya pamoja kati ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang' Mhe. Rose Kamili na wawezeshaji kutoka TGNP, TAWSANET na WaterAid, baada ya kufunga mafunzo ya wanawake viongozi mjini Hanang'

 

Thursday, September 12, 2024

TGNP Empowers Religious Leaders to Champion Women's Leadership

 TGNP Empowers Religious Leaders to Champion Women's Leadership



By Deogratius Koyanga, Mtwara

The Tanzania Gender Network (TGNP) has conducted training programs for religious leaders to empower them to advocate for women's leadership and gender  equality.

As part of the "She Leads" or “mwanamke Ongoza” project, these trainings aim to break down barriers that have traditionally limited women's participation in politics. The project is a joint effort by TGNP and the Aga Khan Foundation, supported by the Canadian government.

With Tanzania's upcoming local government elections, these trainings are particularly timely. They seek to inspire more women to run for office and create a more inclusive political landscape.

Pastor Michael Namakwana of the Mtwara Baptist Church highlighted the crucial role of religious leaders in promoting gender equality. He emphasized the need for these leaders to educate their communities and encourage women to participate in the political process.

Sheikh Yusuf Salum Mwandewa, a Muslim leader from Mkunwa ward, called on political parties to ensure equal opportunities for women candidates. He urged them to avoid discouraging women from running for office or forcing them into special seats positions.

Celestine Lukanga, chairman of the Catholic Church's Dihimba outstations - Mkunwa Parish, stated that the church will actively promote gender equality and combat gender-based violence. They will educate their members and develop strategies to protect women and children.

Through these training programs, TGNP is working to equip religious leaders with the knowledge and tools to become powerful advocates for women's rights. By empowering these leaders, TGNP aims to create a more inclusive and equitable society.