Global Peace Foundation waendelea kutoa elimu ya Amani Mikoa ya Kusini
Na Mwandishi Wetu
Shirika la Global Peace
Foundation Tanzania Kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu -kazi vijana na
Ajira, Chama cha Skauti Tanzania, Taasisi ya Mwalimu Nyerere, GRCF na Vijana Wa
Umoja wa mataifa (YUNA), kupitia program ya Vijana na amani255 inatoa mafunzo
ya Amani Wilaya ya Nyasa yenye lengo la kuhamasisha ushiriki na ushirikishwaji
wa Vijana katika Ujenzi wa Amani kwenye jamii.
Kaimu Mkuu wa wilaya ya Nyasa, Aziza Mangosongo, akitoa hotuba ya ufunguzi |
Mafunzo haya yanatolewa katika
Ukumbi wa Bay live mjini Mbamba bay Kwa Vijana, viongozi wa dini, Viongozi wa
Utamaduni,wazazi walezi, Viongozi wa Serikali na Vijana.
Akifungua mafunzo hayo Kaimu Mkuu
wa Wilaya ya Nyasa Mh Aziza Mangosongo amewataka vijana na wananchi Kwa ujumla
kuwa wazalendo na kudumisha Amani Kwa kufanya kazi Kwa juhudi, na kuilinda
Amani Kwa kuwa Haina mbadala.
Mgeni rasmi, Kaimu Mkuu wa Wilaya katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa mafunzo |
Ameongeza kuwa wananchi wa nchi
ya Tanzania hatuna sehemu nyingine tutakayoishi Kwa amani kama Tanzania, hivyo
ni wajibu wa kila mmoja wetu kuijenga, kuilinda na kuitunza amani yetu.
Amelipongeza shirika Hilo Kwa
kutoa mafunzo haya katika Wilaya ya Nyasa Kwa kuwa Wilaya hii inapakana na Nchi
ya Msumbiji na Malawi hivyo ni elimu Muhimu.
Kwa upande wake Joseph Malekela,
Afisa kutoka Global Peace Foundation, akizungumza kwaniaba ya Mkurugenzi Mkaazi wa Global Peace Fouandation
, Bi. Martha Nghambi alisema kwamba Mradi huo
unatekelezwa katika mikoa mitatu ya Kusini mwa nchi ambayo ni Lindi,
Mtwara na Ruvuma chini ya ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), na kutekelezwa na wadau wenza ambao ni
Ofisi ya Waziri Mkuu (Vijana, Kazi na watu wenye Ulemavu), Chama cha Skauti Tanzania (TSA), Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Asasi ya
Vijana ya Umoja wa Mataifa (YUNA), na Shirika la Global Religions for Children
Foundation (GRCF).
No comments:
Post a Comment