Na
Mwandishi wetu
Vituo vya Taarifa na
Maarifa chini ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Mkoa wa Mara hivi karibuni viliamua
kufanya kampeni ya kupinga ukeketaji ili kupunguza wimbi kubwa la watoto wa
kike kukeketwa kama mila za kikurya zilivyo.
Baadhi ya wasichana wa Kata ya Nyakonga, Wilaya ya Tarime walioshiriki katika kampeni ya kutokomeza Ukeketaji iliyoendeshwa na Kituo cha Taarifa na Maarifa, Nyakonga
Viongozi wa Kituo cha Taarifa na Maarifa wakiwa na wadau wengine wakati wa Kampeni ya kuzuia Ukeketaji
Jamii hiyo ambayo
imejengewa uwezo na TGNP, ilifanya tathimini na kugundua kwamba, kuna koo
ambazo zinakeketa watoto wa kike kila mwaka unaogawanyika kwa mbili, na koo
nyingine zinakeketa mwaka ambao haugawanyiki kwa mbili.
Hivyo katika mwaka huu
ukeketaji unatarajiwa kufanyika mwezi Dec 2022 ambapo wanavituo waliamua kutoa
elimu kupitia mbinu mbalimbali katika kampeni ya kupinga ukeketaji.
Vituo vya Taarifa na
Maatifa vilitumia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha wanawafikia watu wengi kadri
inavyowezekana. Baadhi ya mbinu hizo ni:-
LIGI YA MPIRA WA MIGUU WA
WATOTO WA KIKE
Kituo cha Taarifa na
Maarifa kata ya Nyakonga na Regicheri walifanya bonanza fupi la ligi ya mpira wa
miguu kwa watoto wa kike, ambapo ligi hiyo ilichukua muda wa wiki moja (siku 7) ligi ilikuwa
ikiambatana na elimu mbalimbali juu ya ukatili wa kijinsia ikiwemo na
ukeketaji.
Washindi wa Kombe za kampeni ya kutokomeza Ukeketaji Tarime baada ya kupokea zawadi yao ya Mbuzi
Wanavituo walitumia mifuko
ya vituo ambao inatokana na mapato mbalimbali ya miradi tuliyonayo kwenye vituo
vyetu pamoja na michango mbalimbali ya
wanakituo na wadau mbalimbali, zikanunuliwa zawadi mbalimbali kama vile
mbuzi, kuku, soda, maji nk kwa ajili ya kutoa zawadi kwa washindi wa ligi hiyo.
Wazee wa mila na koo wakiwa wanasikiliza kwa makini mafundisho yaliyokuwa yakitolewa wakati wa michezo na mikutano mbalimbali ndani ya kata ya Nyakonga
Ligi hiyo ilianza Septemba 27, 2022 na
kumalizika Oktoba 04,2022 ikafanyika fainali na washindi kupewa zawadi zao.
Jedwali hapo chini
linaonyesha walionufaika na bonanza hili
kwa kupata elimu juu ya ukeketaji.
|
KITUO |
Watoto wa kike |
Watoto wa kiume |
Watu wazima |
jumla |
|
|
KE |
ME |
||||
|
NYAKONGA |
314 |
211 |
43 |
64 |
632 |
|
REGICHERI |
127 |
89 |
38 |
51 |
305 |
|
JUMLA |
431 |
300 |
81 |
115 |
937 |
Kati ya watoto wa kike waliofikiwa na elimu hii ni 431
kati yao watoto 217 wapo katika hatari
kubwa ya kufanyiwa ukeketaji Dec mwaka
huu 2022.
MIKUTANO YA WANAUME PEKEE NA WANAWAKE PEKEE
Ilifanyika mikutano ya
wanawake pekee, hii ilisaidia kujua kwa undani kwa nini ukeketaji unaendelea
katika jamii zetu, hivyo elimu ilitolewa
kwa wakina mama hao, ambapo jumla ya wanawake 82 walipata elimu hiyo.
Pia ilifanyika mikutano ya
wakina baba ambapo wakina baba walikuwa huru kujieleza ni kwa nini ukeketaji
unafanyika, wengine walijibu kuwa ni tama za baadhi ya wazazi kuwaodhesha
watoto wao na kupata ng’ombe nyingi, wengine walisema ni mazoea ya mila na
desturi na wengine walisema mtoto akikeketwa analeta heshima kwenye familia
zao. Hivyo sisi kama wanakituo tulitoa elimu ya madhara ya ukeketaji na
kuwasihi kubadili mitazamo yao ili kutengeneza jamii yenye mtazamo chanya.
Jumla wa wanaume waliopata elimu hii walikuwa
64
|
KITUO |
WANAUME |
WANAWAKE |
JUMLA |
|
NYAKONGA |
64 |
82 |
146 |
|
|
|
|
|
Baada
ya kampeni hii kukamilika tuliandaa mpango kazi ambao utatuongoza katika
kuhakikisha elimu inawafikia watu wengi zaidi ili wanajamii waweze kubadilika
na kuacha ukeketaji.
CHANGAMOTO
Pamoja
na jitihada zote tulizozifanya bado
tulikuwa na baadhi ya mapungufu katika kutekeleza majukumu yetu hasa upande wa
kipato hakikuwa cha kutosha kuweza kufanya vitu vikubwa zaidi. Lakini pia
tunaomba upande wa TGNP iweze kutupa nguvu zaidi katika kupambana na ukeketaji
katika jamii zetu hasa semina/warsha/matamasha madogomadogo ya mara kwa mara yakiwashirikisha viongozi wa serikali, viongozi wa mila na
viongozi wa dini, pia kuna baadhi ya wavituo wanaotakiwa kujengewa uwezo zaidi
katika mapambano haya dhidi ya
ukeketaji.
No comments:
Post a Comment