Wednesday, May 29, 2024

TWCC yawataka wanawake kujitokeza uchaguzi serikali za Mitaa

TWCC yawataka wanawake kujitokeza uchaguzi serikali za Mitaa

Na Deogratius Temba; Chamwino

Mkurugenzi Mtendaji, TWCC, Ms. Mwajuma Hamza, akizungumza na washiriki wa mafunzo ya Uongozi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Chamwino, Mkoani dodoma, yaliyowahusisha wanawake kutoka kata 18 za Wilaya hiyo.


WANAWAKE wametakiwa kujiimarisha kiuchumi kwa kuwekeza kwenye miradi mikubwa na kushiriki kwenye nafasi za uongozi na maamuzi katika ngazi mbalimbali ili kubadili mfumo itakayoweka mazingira wezeshi kwa wanawake kufanya biashara

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Chemba ya Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), Mwajuma Hamza, wakati wa kufunga mafunzo ya wanawake viongozi yanayolenga kuongeza kasi ya kuwezesha wanawake vijiji ni, na kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi wa serikali za Mitaa mwaka huu 2024, yanayofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino , Mkoani Dodoma.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mradi wa kuongeza kasi ya uwezeshaji wanawake vijijini, unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Wanawake (Unwomen) unaotekelezwa katika wilaya ya Chamwino.

“wilaya ina kata 36, madiwani wanaume ni 35 na mwanamke Diwani wa kata ni mmoja pekee, vijiji 107 lakini mwanamke mwenyekiti ni mmoja pekee. Hii sio sawa, hakuna usawa wa Kijinsia katika uongozi, tunahitaji mabadiliko makubwa katika eneo hili. Tuongeze wanawake viongozi tafadhali” alisema Mwajuma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TWCC, Mercy Silla, alisema kwamba, wanawake wanatakiwa kumiliki uchumu wa viwanda vikubwa na miradi mingine mikubwa ili kujikwamua kiuchumi, kubadilisha kaya zao kiuchumi na kujiwezesha kiuchumi ili waweze kugombea nafasi za uongozi

“Tunataka wanawake wamiliki miradi mikubwa yenye fedha. Kugombea uongozi unahitaji fedha na unahitaji kuwa vizuri kiuchumi, familia za viongozi ni lazima ziwe na ustawi, ndio maana TWCC tunasisitiza, wanawake wafanyabiasha kuboresha biashara zao, na kuhakikisha wanajitokeza kugombea nafasi za uongozi sambamba na kuingia kwenye nafasi za maamuzi ili wakabadilishe sera ambazo haziwapi nafasi wanawake kuwa wawekezaji au wafanyabsiahara wakubwa”alisema Sila.

Lakini pia amesema kwamba, wanawake watakapokuwa kwenye uongozi watapata nafasi ya kutoa elimu na kubadilisha mitazamo hasi, mila na desturi kandamizi  zilizoko kwenye jamii juu ya uwezo wa wanawake viongozi

Mafunzo hayo yamewezeshwa na Deogratius Temba, ambaye ni mtaalam na mkufunzi wa masuala ya Jinsia na uongozi, na kuwajumuisha viongozi wanawake kutoka katika ngazi ya Kitongoji, ujumbe wa serikali za Mitaa, kamati na bodi mbalimbali na madiwani wanawake kutka kata 18 za mradi huo.









Saturday, March 9, 2024

TGNP yawapiga msasa viongozi wanawake Kondoa

 TGNP yawapiga msasa viongozi wanawake Kondoa


Na Mwandishi wetu

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) wamefanyamafunzo ya kujenga uwezo wa uongozi na kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafsi za uongozi na maamuzi

Mafunzo hayo ambyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Mwanamke Ongoza  unaotekelezwa na  TGNP kwa kushirikiana na Taasisi ya Aga Khan Foundation na Serikali ya watu wa Canada, unaolenga kujenga uwezo kwa viongozi wanawake walioko madarakani ili kuboresha utendaji wao kwa manufaa ya jamii na kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi.

Pia mradi huu, unataka kuondoa vikwzo vinavyo wafanya wanawake waliopewa dhamana ya uongozi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi ipasavyo, ambavyo ni pamoja na shughuli za huduma na matunzo kama vile utafutaji wa maji, shughuli za nyumbani, kuhudumia wagonjwa na utunzaji wa watoto ambazo zinaweza kufanywa na mtu mwingine kwenye familia, ikiwa ni sambamba na kubalisha mitazamo, mila na desturi na tamaduni zilizopitwa na wakati ambazo zinakwamisha wanawake kushiriki kwenye uongozi.

Kwa upande wake, Diwani wa Viti maalum Halmashauri ya wilaya ya Kondoa, Madina Fentu, alisema kwamba, mradi huu umemsaidia kwa kiasi kikubwa kupata uelewa wa mambo mengi lakini pia mume wake ameweza kushiriki moja ya semina ambazo alinufaika nazo.

“kwa kweli, ile warsha wa wenza wa viongozi wanawake imetusaidia sana, wenza wetu waliposhiriki, tumeona mabadiliko, pamoja na kwamba mimi mume wangu alikuwa akinisaidia awali, lakini aliongeza sana kunisaidia, hasa pale ninapokuwa na majukumu mengi ya kiuongozi na kushindwa kuhudumia familia” alisema Madina

Mapendekezo yaliyotoka kwenye warsha hiyo ni pamoja na Halmashauri zianzishe kanuni ya utaratibu wa kuwatangaza wanawake viongozi wa mfano wa kuigwa  na jamii na wapewe nafasi ya kuonekana ili kubadilisha mitazamo hasi kwa jamii kwamba wanawake hawezi kuwa viongozi wazuri.

Kutoa elimu ya kubadilisha mitazamo hasi kwa viongozi wa dini zote, wazee wa mila, wazee maarufu ili wawe mstari wa mbele katika kubadilisha mitazamo hasi, Kuweka kanuni kali za kutokomeza Ukatili wa Kijinsia, Udhalilishaji wa kijinsia wakati wa chaguzi, sambamba na kuendelea kuwaelimisha wanaume ili kuwasaidia wenza wao ambao ni viongozi wa kisiasa katika majukumu ya kifamilia ili waweze kuhsiriki vizuri kwenye majukumu yao.

Viongozi wanawake walioshiriki mafunzo hayo ni Madiwani  wa Kata, madiwani wa viti maalum, Wenyeviti wa Vitongoji, wajumbe wa serikali za Vijiji, viongozi wa vyama vya siasa, na viongozi wataalamu ngazi ya jamii.  

 


















Tuesday, March 5, 2024

TGNP yawapiga msasa wadau na viongozi wanawake Dodoma

 TGNP yawapiga msasa wadau na viongozi wanawake Dodoma

Na Mwandishi Wetu, Kondoa

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Imewajengea uwezo wadau mbalimbali kutoka kwenye mashirika, asasi na vikundi vya kijamii kuhusu namna ya kuongeza Ushiriki wa Wanawake ngazi za uongozi na maamuzi Halmashauri ya Wilaya Kondoa Mkoani Dodoma

Mafunzo haya yanatolewa katika Halmashauri za Wilaya ya Kondoa,Morogoro na Mtwara, kama sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa ‘’Mwanamke Ongoza-She Leads’’ unaotekelezwa na TGNP kwa ufadhili wa Agakhan Foundation na Serikali ya Watu wa Canada unaolenga kuwezesha wanawake viongozi walioko madarakani kutekeleza majukumu yao vizuri ya kiuongozi na kuongeza ushiriki Zaidi wa wanawake kwenye nafasi za uongozi na maamuzi.



Mafunzo hayo yamewanufaisha jumla ya washiriki 30 ambao ni viongozi wa vikundi vya Bodaboda, Dini, vikundi vya kijamii, asasi za kiraia, watu maarufu wenye ushawishi, ambao baada ya mafunzo hayo wataenda kutoa elimu kwenye vikundi vyao na kushawishi wanawake kushiriki kikamilifu kwenye nafasi za maamu.

Mwezeshaji mwenza kutoka TGNP, Ester Wiliam alisema kwamba warsha hiyo inalenga  kuongeza uelewa wa dhana za jinsia na uongozi,ubainishaji wa fursa zilizopo katika mifumo ya vyama na kwenye jamii ili kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi,

Ameongeza kwamba washiriki hao, wamejengewa uwezo kubainisha na kuchambua  mifumo kandamizi inayomzuia mwanamke kushiriki katika nafasi za uongozi na ngazi za maamuzi. 

“Mafunzo haya yanaenda kuongeza nguvu kwenye Tapo, kwasababu hawa tuliowajengea uwezo wanatoka kwenye makundi mengi, taasisi ndogondogo zinazofanya kazi katika kata ya Haubi, ambapo wakienda kupeleka ujumbe tutakuwa tumewafikia watu wengi sana” alisema Esther

Kwa upande wake Anna Ambrose, Katibu wa Kituo cha Taarifa na Maarifa Haubi, amesema kwamba, mafunzo hayo yanaenda kubadilisha mitazamo ya jamii katika uwezo wa wanawake kuwa viongozi, lakini pia kubadilisha baadhi ya mila na desturi zinazokwamisha wanawake kuwa viongozi katika jamii hiyo.
















 

Tuesday, February 20, 2024

TGNP and LGTI -Hombolo conduct training on Gender to LGA Officials at Ward Level


Participants group photo 

By Deogratius Temba,Dar

Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) in collaboration with the Local Government Training Institute (LGTI) Hombolo, supported by UNWOMEN Tanzania through the Women Leadership and Economic Rights Project (WLER), have officially kicked off a four days training to Local Government officials at ward level on Gender Mainstreaming and Gender Responsive Budgeting. 

The training is being carried out in Dar es Salaam involving officials at the ward level from Lindi, Mtwara and Dar es Salaam regions.

The Women Leadership and Economic Rights Project (WLER) is currently being implemented in various regions to promote women’s participation in leadership and the right to benefit from economic opportunities.


Ms. Lilian Liundi, The Executive Director, Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) during the Opening session in Dar es salaam


Dr. Lazaro Kisumbe, Deputy Rector LGTI- Hombolo during the opening session


Speaking during the official opening, Lilian Liundi, TGNP’s Executive Director said that, this training is a great opportunity for capacity strengthening of council officials that will help them understand how to effectively engage community members in the government planning processes at ward and village levels.

“This training resulted from the realization that; LGA officials need to understand gender issues and have them prioritized at community level during planning. This together alongside collaboration with the community members themselves will help in managing the O&OD process which will consequently be beneficial to the communities they serve said Liundi

She also added that, due to their importance and the positions they have at the community level, the participants of the training have the ability to provide education in the community through township and village meetings to make women participate but also to come forward to run for leadership to increase the number of women in positions leadership and decisions at the village and local level.

On the other hand, the Deputy Rector- Adminisitration and Finance of the Local Government Training Institute (LGTI) Dr. Lazaro Kisumbe who was also the guest of honor in the official opening of the training said that, the Institute had carried out research which identified several existing gender gaps in the Local Government Authorities which hinder government efforts in planning and budgeting with a Gender perspective.

“The WLER project intends to close the existing gender gaps which is the reason why with the support from UNWOMEN Tanzania, we are collaborating with TGNP to capacitate ward level local government officials who will then go back to their duty stations to share and enlighten their respective Ward.

Development Committees on how to mainstream gender during planning processes while incorporating community priorities,” he said.

He also added that, through this training, officials will be able to identify ways that gender can be

mainstreamed at the ward level and also ensure that the concept of gender and issues related are well understood at all levels.