Sunday, February 9, 2025

NAFASI YA MWANAUME KATIKA KULEA WATOTO NJITI

 NAFASI YA MWANAUME KATIKA KULEA WATOTO NJITI

·     Malezi ya Kangaroo yanahitaji wanaume kushiriki

·     Baadhi ya wanaume hulazimika kufunga biashara, kulea

·     Likizo ya uzazi kwa wanaume yashauriwa


Deogratius Temba, Mwandishi wa makala hii akizungumza na Ndugu Mohamed, wakati wa mahojiano maalum


Na Deogratius Temba

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ipo katika mchakato wa kufanya marakebisho kwenye sheria kuu ya Ajira  na mahusiano Kazini, sura ya 366, ambapo moja ya kifungu cha sheria hiyo kinachofanyiwa marakabisho ni pamoja na kuongezwa kwa muda wa likizo kwa wanawake wanaojifungua watoto njiti.

Kifungu kinaeleza kwamba Mama aliyezaa motot njiti ataendelea kuwa likizo yenye malipo hadi zitimie wiki ya 36 ya ujauzito na baadaye aendelee na likizo yake ya uzazi kama kawaida.

Katika mswada huo, marakabisho yanafanyika kwenye sheria ya msingi ya awali kwamba: Kifungu cha 33 cha muswada kinaeleza kwamba “  Sheria inarekebishwa katika kifungu cha 33 kwa- (a) kuongeza mara moja baada ya kifungu kidogo (7) yafuatayo: "(8) Mfanyakazi anayezaa mtoto kabla ya muda wake ana haki ya likizo ya uzazi iliyolipwa kuanzia tarehe ya kujifungua hadi kukamilika kwa wiki thelathini na sita za ujauzito na hadi kipindi cha likizo ya uzazi kilichotolewa chini ya kifungu kidogo (6) katika mzunguko wa likizo.";

Inaelezwa kwamba, lengo la marekebisho haya ya sheria, sio upendeleo tu kwa wanawake, bali inalenga kulinda ustawi wa afya za watoto wanaozaliwa kabla ya wakati na kuhitaji muda wa kutosha wa aungalizi wa mama na Baba.  Mtandao wa Haki ya Afya ya Uzazi (SRHR), unaoratibiwa na Mfuko wa Wanawake Tanzania (WFT-T) wanapendekeza kuwepo kwa likizo ya kutosha ili kuhakikisha kwamba wanawake na wanaume wanapata nafasi ya kumlea mtoto njiti bila tatizo.

Mtandao wa Haki ya Afya ya Uzazi, wakiongozwa na shirika la Doris Moleli Foundation, Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi (TUCTA),  chini ya usimamizi wa WFT-T wanasema kwamba, ili kuongeza tija katika uzalishaji mali nchini na kujenga taifa la wetu wenye afya njema na nguvu kazi ya baadaye ni lazima kulinda afya na ukuaji wa watoto njiti.

“Kifungu kina tija kwa wafanyakazi waliojifungua kabla ya muda ili kuruhusu mzazi kuhudumia mtoto kwa ukaribu ili atengemee isipokua siku zilizotajwa hapo ziongezeke kutoka wiki 36 mpaka wiki 40 kwa sababu za Kiafya hasa makuzi ya mtoto” linasema moja ya pendekezo la Mtandao huo kwa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii waliowasilisha kuhusu muswada huo.  Mtandao wa SHRSR, TUCTA na wengine wanapendekeza kwamba  likizo ya malipo ya wiki za kabla ya kujifungua ambazo mama angekuwa hajajifungua ziongezeke hadi wiki 40 kwasababu wanawake wengi hujifungua kati ya wiki ya 36 hadi 40 na ndipo ianze likizo rasmi ya uzazi.

Likizo inayopendekezwa ni kwa wanawake (Mama anayejifungua) na mume wake kwasababu za msingi ambazo ni kwamba, mtoto njiti anahitaji malezi ya pande zote na pia Mama aliyejifungua anahitaji usaidizi wa mwenza wake wakati huu.

Kwa mujibu wa sheria kuu ya ajira na mahusiano kazini nchini Tanzania, sura ya 366, vifungu 33  na 34 vinavyozungumzia likizo za watumishi, hakuna kabisa suala la likizo ya mama anayejifungua mtoto njiti, lakini kutokana na marekebisho haya yam waka 2025, kwa mara ya kwanza Tanzania itakuwa imegusia suala la mtoto njiti kwenye sheria.

Kifungu cha 34 cha sheria n ahata kwenye muswada,  hakielezi kuhusu likizo ya uzazi kwa wanaume ambao wenza wao wanajifungua watoto njiti, hii inamkosesha baba nafasi ya kushiriki katika kumhudumia mtoto wake au  kumsaidia mwenza wake jukumu ya akulea.

Jambo la msingi la la kiafya kwa mtoto aliyezaliwa Njiti, ni kutunzwa kwa mfumo wa Kangaroo, ambao unamuhitaji mama kumweka mtoto kifuani muda wote ilia pate joto la mwili badala ya kutumia mashine ambazo ni gharama kubwa katika hospitali. Mama anayejifungua mtoto njiti anaweza kuruhusiwa kutoka hospitalini mapema na akakaa nyumbani na mtoto wake endapo atakuwa na usaidizi wa Baba wa mtoto katika kumsaidia kumweka mtoto kifuani (Kangaroo).

Utaratibu wa Kangaroo ulipendekezwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 1978 na madaktari wa watoto wawili katika kitengo cha uzazi katika Hospitali ya San Juan de Dio huko Bogotá, Colombia. Leo hata Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema njia hii ni bora zaidi.

Mohamed Saleh, ni Mume wa Dada Saada Nassor Mohamed, wakazi wa Dar es salaam nchini Tanzania ambaye amezaa watoto wawili (2)  kabla ya muda (njiti), Mohamed analeza jinsi avyowajibika kumsaidia mke wake katika malezi ya mtoto njiti ili kukoa maisha ya mtoto  lakini pia kupunguza gharama ambazo zingelipwa hosipitalini.

“tulipitia kwenye kipindi kigumu kwa babu tulipata mtoto njiti,gharama za Hopsitali zilikuwa kubwa, matunzo ya mtoto wodini ni Zaidi ya shilingi  200,000 kwa siku, lakini tulishauriwa kuondoka Hospitalini na tukatumia mfumo huu wa kangaroo, ambapo Mimi kama (Baba) nililazimika kusaidia mke wangu kumweka mtoto kifuani ilia pate joto”

Wakati mke wangu anajifungua hawa watoto Njiti, hasa huyu wa mwisho, nilitoa muda wangu mwingi, ilinilazimu kufunga biashara ili nikae nyumbani kumsaidia mke wangu kumtunza mtoto. Wakati tunaruhusiwa kutoka Hospitalini tulipewa masharti endapo tunataka mtoto apone, basi, asishikwe na mtu mwingine yeyote isipiokuwa mimi na Mama. Niliamua, ili mtoto apone na kukua, ni lazima nitumie muda huo kumlinda na kumtunza kwa kuzingatia masharti ya kulea mtoto njiti” anasema Mohamed

“ mfumo wa Malezi ya Kangaroo, una gharama kubwa, nililazimika kuacha kazi kwa miezi 4, nikafunga biashara zangu ili nipate muda wa kumlea mtoto apate joto na kukua”  anaongeza Mohamed.

Mohamed anawaasa wanaume wote kuwa karibu na wenza wao hasa wakati wa ujauzito, kuhakikisha malezi ya mimba ni ya wote, lakini pia wanawake wanapo zaa watoto njiti wasitengwe au kufanyiwa ukatili au kutelekezwa. “Nafasi ya Baba ni muhimu sana ili kuwa na mtoto mzuri mwenye afya njema. Mwanaume akishiriki kumtunza mtoto ataokoa gharama za matibabu, kwasababu mtoto hatapatwa na maambukizi” anaongeza Muhamed

Kwa upande wa Bi. Saada Nassor Mohamed, akizungumzia mchango wa Mume wake  wakati alipojifungua mtoto njiti anasema “ nilipojifungua mtoto njiti, kwanza sikuamini, nilipoona mtoto hana hata  umbo nzuri, nilistuka sana, nikamwambia daktari kwamba amenibadilishia mtoto, nilimuita mume wangu na kumweleza. Lakini alipofika alinitia moyo, alikaa na Daktari wakaelewana wakaniweka vizuri. Mume wangu tangu siku hiyo hakuniacha mbali, aliacha shughuli zake, akaanza kunisaidia katika malenzi ya Kangaroo, Nimeona mchango mkubwa sana wa Mume wangu” anasema Bi. Saada.

Kwa upande wake Mkurugrenzi Mtendaji wa Mfuko wa Wanawake (WFT-T) Tanzania, Bi. Rose Marandu, anasema kwamba changamoto ya uzazi wa kabla au kuzaa mtoto njiti  ni kubwa,  na linahitaji kuwekewa kipaumbele na serikali katika kutenga rasilimali fedha ili kuboresha huduma za afya, kuweka fedha kwaajili ya kuboresha huduma kwenye zahanati na vituo vya afya vijijini ili kuwezesha wanawake masikini wa vijijini kutokuhangaika kusaifiri mbali kufuata huduma katika hospitali kubwa.



Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Moleli, Foundation, Bi. Doris Moleli anasema kwamba, yeye alizaliwa mtoto njiti na kwa jinsi alivyoona changamoto wanazokumbana nazo wanawake wanaozaa watoto njiti, ameamua kujikita katika kupigania haki na kuteteza huduma za afya hasa kwa uzazi wa watoto njiti ziboreshwe.

Sizya Puya ni Mama wa watoto Njiti, ambapo kila uzazi aliopitia alipata mtoto njiti, na ameweza kulea  vizuri kwa kuzingatia masharti ya kulea na watoto wake wana afya njema na wanaendeela na masomo.

Sizya anaeleza kwamba, nafasi ya Mzazi wa kiume ni muhimu sana, kwa kuzingatia mahitaji ya kumelea mtoto njiti ni makubwa. “kuna suala la rasilimali fedha, inahitaji fedha kuanzia nyumbani kuboresha mazingira na usafi wa kila kitu, lakini gharama za matibabu, dawa, sindano, usafiri wa kwenda hospitalini na kurudi, lakini pia usaidizi wa nyumbani hasa mama anapokuwa anashinda ya kiafya kama maumivu ya mgongo, Baba atahitajika kumsaidia kumbeba mtoto” anaeleza Sizya.

Doris anasema kwamba “…Imetokea mara kadhaa wanawake wana acha kazi au kuachishwa kutokana na uzazi, mwaka 2017 tulianzisha hii agenda ya kuomba serikali iongeze siku za uzazi kwa mama anayejifungua mtoto njiti, mwaka  2018 tulishawishi wizara iongeze siku za likizo ya uzazi kwa  wanaume, lakini haikufanikiwa. Mwaka 2019, tuliamua kuunganisha nguvu kwa kiasi kikubwa na wadau wengine wengi Zaidi.  Baadaye WFT-T ilitusaidia kuunganisha nguvu na kuunda Mtandao wa SRHR ambapo tulipata  nafasi ya kuwa na sauti ya pamoja katika kupigania haki za wanawake na sasa tumefikia mafanikio ya kupata kifungu cha sheria.

No comments:

Post a Comment