Wednesday, December 7, 2022

TGNP YATOA MAFUNZO KWA AZAKi ZINAYOTETEA HAKI ZA WANAWAKE NA USAWA WA KIJINSIA

 


 Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umeandaa mafunzo ya kuimarisha uwezo 

wa ushawishi na uchechemuzi kwa mashirika yanayotetea haki za mwanamke na

 usawa wa kijinsia yaliyoanza leo 

Desemba 06 hadi 09, 2022 yakiwa na lengo la kuongeza uelewa wa dhana ya

 kijinsia, kuongeza ujuzi wa washiriki wa ushawishi na 

uchechemuzi wa masuala ya kijinsi, kutambua fursa zilizopo kwa ajili ya kuwezesha

 uchechemuzi ngazi ya Serikali pamoja na 

kuandaa mikakati na mipango kwa ajili ya kujega sauti na utendaji wa pamoja

 na katika ushawishi na uchechemuzi wa masuala

 ya kijinsia.


Akizungumza Mwezesha wa Mafunzo hayo Mary Nsemwa amesema washiriki wa 
mafunzo haya ni wadau mbalimbali kutoka Taasisi mbalimbali  zunazoshughulikia 
masuala kijinsia pamoja na haki za wanawake 
hivyo wamekutanishwa hapa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) ili kuwaongezea 
uelewa kuhusu masuala ya kijinsia ili 
waweze kuongeza ushawishi zaidi kwenye jamii.

Amesema Suala la ukatili wa kijinsia linatokea kwasababu nyingi lakini ukiangalia
 nyuma ya hili ni kuwa ukatili wa kijinisa umebeba nguvu na mfumo duni kwasababu
  anayefanya ukatili anajiona yeye ndo 
mwenye nguvu kuliko anayemfanyia ukatili mfano ukatili wa mwanaume kwa 
mwanamke hii ni kutokana na Mwanume kujiona 
yeye ana nguvu  na hata jamii pia inamuona ni mtu wa tofauti au mwanamke kwa mtoto
 kwasababu yeye anauwezo wa 
kufanya chochote kwa mtoto wake.

pia amesema wadau hawa wakijengewa uwezo na kujenga sauti ya pamoja ya kukemea
 masuala yote ya ukatili wa kijinsia watakwenda kujenga msingi mzuri hasa kutengeneza
 vuguvugu na nguvu zaidi kwenye suala
 la kupunguza ukatili wa kijinisia maana zikiachwa ziendelee zitakuja kuleta madhara 
makubwa baadae kwenye jamii na 
hasa zitamuumiza sana Mama na mtoto.

Naye mnufauka wa mafunzo Selina Lyapinda ameushukuru Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP

) kwa kuweza kuwapa mafunzo hayo kwani yatawaongezea uelewa kwenye masuala 

ya kijinsia na kupambana na masuala haya kwenye jamii ambayo yamekidhiri.

\
Mwezesha wa Mafunzo Mary Nsemwa akiwasilisha mada iliyokuwa inahusu dhana 
za Jinsia na maana yake katika muktadha wa sasa wakati wa mafunzo ya 
kuimarisha uwezo wa ushawishi na uchechemuzi kwa mashirika yanayotetea
 haki za mwanamke na usawa wa kijinsia yaliyoanza leo Desemba 06 hadi 09, 2022 
yakiwa na lengo la kuongeza uelewa wa dhana ya kijinsia yaliyoandaliwa na Mtandao 
wa Jinsia Tanzania (TGNP) yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwezeshaji wa Mafunzo hayo Deo Temba akiwasilisha mada kuhusu kuongeza
 ujuzi wa washiriki wa ushawishi na uchechemuzi wa masuala ya kijinsi na kijinsia 
wa mafunzo ya kuimarisha uwezo wa ushawishi na uchechemuzi kwa mashirika
 yanayotetea haki za mwanamke na usawa wa kijinsia yaliyoanza leo 
Desemba 06 hadi 09, 2022 yaliyoandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) 
yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wakichangia mada zinazohusu namna ya kuongeza
 kuongeza ujuzi wa washiriki wa ushawishi na uchechemuzi wa masuala ya 
kijinsi na namna ya kuongeza uelewa wa dhana ya kijinsia kwa mashirika
 yanayotetea haki za mwanamke na usawa wa kijinsia wakati wa mafunzo
 yalioandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) yaliyoanza leo Desemba
 06 hadi 09, 2022.
Baadhi ya washiriki wakijadiliana kwenye makundi  ili kuongeza kuongeza ujuzi 
wa washiriki wa ushawishi na uchechemuzi wa masuala ya kijinsi na namna ya 
kuongeza uelewa wa dhana ya kijinsia kwa mashirika yanayotetea haki za
 mwanamke na usawa wa kijinsia wakati wa mafunzo yalioandaliwa na Mtandao
 wa Jinsia Tanzania (TGNP) yaliyoanza leo Desemba 06 hadi 09, 2022.

No comments:

Post a Comment