TGNP yawanoa viongozi wa
dini,ushiriki wa wanawake kwenye nafasi za uongozi
Na Deogratius Koyanga, Mtwara
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP)
umefanya mafunzo ya kujenga uwezo kwa viongozi wa dini zote ili waweze
kuhamasiaha ushiriki wa wanawake kwenye nafasi za uongozi
Mafunzo hayo ambayo ni sehemu ya
mradi wa “mwanamke Ongoza’ unaotekelezwa na TGNP kwa ushirikiano na Taasisi ya
Aga khan Foundation kwa ufadhili wa serikali
ya watu wa Canada, yanafanyika wakati nchi yetu ikielekea kwenye uchaguzi wa
serikali za Mitaa mwaka huu 2024, kukiwa na mkazo kuhusu kushawishi wanawake
wajitokeze zaidi kwenye nafasi za uogozi.
Akiozungumza Mchungaji Michael
Namakwana, wa Kanisa la Bapitist Mtwara
alisema kwamba mafunzo ya viongozi wa dini juu ya usawa wa Kijinsia na ushiriki
wa wanawake kwenye nafasi za uongozi na maamuzi yatawezesha kuleta mabadiliko
makubwa kwasababu baada ya kupata maarifa na uelewa wa masuala ya kijinsia
watatumia majukwaa yote ya kanisa kuhakikisha wananachi wanapata elimu na wanawake wanajitokeza kushiriki kwenye
uchaguzi wa serikali za Mitaa na watashinda.
“sisi viongozi wa dini kwa nafasi
zetu tunaalikwa na viongozi wa serikali pia kushiriki mikutano ya vijiji nay a kata,
tutatumia nafasi hiyo kuzungumzia masuala haya ili ujumbe ufike kwa mapana
yake..” alisema Mchungaji
Kwa upande wa wasilam, sheikh, Yusuf
Salum Mwandewa, kutoka kata ya Mkunwa alisema kwamba viongozi wa vyma vya siasa
wajitahidi kutoa nafasi kwa wanawake wanaotarajia kugombea nafasi badala ya
kuwarudisha nyuma au kuwalazimisha kugombea viti maalum.
Mwenyekiti wa Kanisa Katoliki Kigango
cha Dihimba,Jimbo Katoliki la Mtwara, Selestine
Lukanga alisema kwamba wao watatumia majukwaa yote ya ndani ya kanisa kuanzia
ngazi ya Kigango, hadi jumuiya ndogondogo, hasa wakati wa matangazo kanisani na
kuvitembelea vyama vya kitume vyote kuwapa elimu ya masuala ya kijinsia,
ikiwepo kuweka mikakati ya kuzuia na kutokomeza vitendo vya Ukatili wa Kijinsia
kwa wanawake na watoto.
No comments:
Post a Comment