Na Mwandishi wetu, Kibaha
Wananchi kutoka kata ya Pangani, Halmashauri
ya Wilaya ya Kibaha Mji, wanaoshiriki utafiti wa kiraghibish unaofanywa na
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), wametoa malalamiko ya uwepo wa baadhi ya
viongozi wa serikali za Mitaa wanaodai rushwa ya ngono kwa wanawake ili waweze
kuwasaidia kupata huduma ya urasimishaji ardhi kwa bei nafuu.
Wakiwasilisha matokeo ya utafiti
raghibish uliofanywa na Jamii hiyo, wakati wa mrejesho ngazi ya Halmashauri kama
sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa “ Uimarishaji wa Sauti za wanawake, wasichana
na watu wenye ulemavu katika uongozi na haki ya kumiliki rasilimali”
unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya
wanawake (UNwomen), washiriki hao wapatao 30 walisema kwamba mchakato wa
upimaji na umilikishaji wa ardhi katika kata hiyo yenye mitaa nane umegubikwa
na vitendo vya kuomba rushwa ya pesa na rushwa ya ngono kwa wanawake
“Jamii yenye migogoro haiwezi
kupata ustawi na maendeleo, tunaomba jambo hili liishe kwa kufikia
mawisho.tumebaini kwamba baadhi ya viongozi wanautumia mgogoro huu kuomba
rushwa ya pesa na rushwa ya ngono kwa wanawake ili wawapunguzie gharama za
kulipia upimaji na urasimishaji” alisema Malaki … ambaye alikuwa msoma risala.
Washiriki hao, wakiwasilisha
mapendekezo yao kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Charles
Marwa, wamesema kwamba, pamoja na mapendekezo hayo, pia wameandaa mpango kazi
ambao watautekeleza sambamba na viongozi wao. Kikao kazi hicho kilichoandaliwa
na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya
Jamii wilayani hapo, pia kimehudhuria na wakuu wa Idara na Vitengo wa
Halmashauri hiyo pamoja na Mkuu wa dawati la Jinsia Polisi
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo alistuka kusikia hivyo na
kuahidi kufuatilia mara moja kwa kutuma timu kuchunguza ukweli wa jambo hilo
ili hatua ziweze kuchukuliwa haraka.
“jambo hili la rushwa ni bay asana, tena rushwa ya ngono,
mtu anataka akunyime haki yako tu ilia pate ngono, tunataka tupate ushahidi wa
kutosha wa hili, naomba mtupe ushirikiano ili tulifanyie kazi” alisema Marwa.
No comments:
Post a Comment