TGNP yawapiga msasa viongozi wanawake Kondoa
Na Mwandishi wetu
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) wamefanyamafunzo ya
kujenga uwezo wa uongozi na kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafsi za
uongozi na maamuzi
Mafunzo hayo ambyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa
Mwanamke Ongoza unaotekelezwa na TGNP kwa kushirikiana na Taasisi ya Aga Khan
Foundation na Serikali ya watu wa Canada, unaolenga kujenga uwezo kwa viongozi
wanawake walioko madarakani ili kuboresha utendaji wao kwa manufaa ya jamii na
kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi.
Pia mradi huu, unataka kuondoa vikwzo vinavyo wafanya wanawake waliopewa dhamana ya uongozi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi ipasavyo, ambavyo ni pamoja na shughuli za huduma na matunzo kama vile utafutaji wa maji, shughuli za nyumbani, kuhudumia wagonjwa na utunzaji wa watoto ambazo zinaweza kufanywa na mtu mwingine kwenye familia, ikiwa ni sambamba na kubalisha mitazamo, mila na desturi na tamaduni zilizopitwa na wakati ambazo zinakwamisha wanawake kushiriki kwenye uongozi.
Kwa upande wake, Diwani wa Viti maalum Halmashauri ya wilaya ya Kondoa, Madina Fentu, alisema kwamba, mradi huu umemsaidia kwa kiasi kikubwa kupata uelewa wa mambo mengi lakini pia mume wake ameweza kushiriki moja ya semina ambazo alinufaika nazo.
“kwa kweli, ile warsha wa wenza wa viongozi wanawake imetusaidia sana, wenza wetu waliposhiriki, tumeona mabadiliko, pamoja na kwamba mimi mume wangu alikuwa akinisaidia awali, lakini aliongeza sana kunisaidia, hasa pale ninapokuwa na majukumu mengi ya kiuongozi na kushindwa kuhudumia familia” alisema Madina
Mapendekezo yaliyotoka kwenye warsha hiyo ni pamoja na Halmashauri zianzishe kanuni ya utaratibu wa kuwatangaza wanawake viongozi wa mfano wa kuigwa na jamii na wapewe nafasi ya kuonekana ili kubadilisha mitazamo hasi kwa jamii kwamba wanawake hawezi kuwa viongozi wazuri.
Kutoa elimu ya kubadilisha mitazamo hasi kwa viongozi wa dini zote, wazee wa mila, wazee maarufu ili wawe mstari wa mbele katika kubadilisha mitazamo hasi, Kuweka kanuni kali za kutokomeza Ukatili wa Kijinsia, Udhalilishaji wa kijinsia wakati wa chaguzi, sambamba na kuendelea kuwaelimisha wanaume ili kuwasaidia wenza wao ambao ni viongozi wa kisiasa katika majukumu ya kifamilia ili waweze kuhsiriki vizuri kwenye majukumu yao.
Viongozi wanawake walioshiriki mafunzo hayo ni Madiwani wa Kata, madiwani wa viti maalum, Wenyeviti wa Vitongoji, wajumbe wa serikali za Vijiji, viongozi wa vyama vya siasa, na viongozi wataalamu ngazi ya jamii.