Monday, June 5, 2023

MWALIMU ALIYEKUWA ANAISHI DARASANI AJENGEWA NYUMBA NA WANANCHI

 

SALVATORY NTANDU, Shinyanga

Uwepo wa Vituo vya Taarifa na Maarifa Katika Wilaya ya Kishapu, Mkoani Shinyanga umetajwa kuwa kichocheo muhimu katika ujenzi wa Vuguvugu na mabadiliko chanya kwenye jamii ambapo katika Kijiji cha Miyuguyu, Kata ya Kiloleli,  wilayani Kishapu wamefanikiwa kuhamasisha wananchi kujenga nyumba mpya ya Mwalimu na matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Msingi Miyuguyu.

Mwezeshaji kutoka TGNP akiwa kwenye mazungumzo na baadhi ya wanajamii wa Kijiji cha Miyuguyu wakati wa tathimini ya mafanikio ya Vituo vya Taarifa na Maarifa.


Hayo yamebainishwa katika Kikao cha Tathimini ya hali ya utendaji kazi wa Kituo cha Taarifa na Maarifa katika kata hiyo, ambapo Agness Kwilasa katibu wa kituo hicho, amesema mafanikio hayo yamesababishwa na hamasa iliyotokana na Bunge la jamii lililoendeshwa na Kituo hicho kwa kushirikiana na uongozi wa vijiji katika kata hiyo.

Vituo vya Taarifa na Maarifa huanzishwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwenye ngazi ya Kata, baada ya kufanya uraghibishi ambao huwawezesha wananchi kutambua nafasi yao, kwa kuibua changamoto, kuzichambua na kuweka mikakati ya kuzitatua wakiwa wameshirikiana na viongozi wao ngazi ya kitongoji, kijiji, kata na Halmashauri. Aidha, Vituo hivi hushirikiana na viongozi wa serikali za Vijiji kuendesha Bunge la Jamii ambalo ni seheu ya kujenga mijadala namna ya kututua changamoto hizo.

Jengo la matundu 12 ya vyoo ambayo jamii ya kijiji cha Miyuguyu walishirikiana na viongozi na wadau wengine kuyajenga baada ya kujengewa uwezo na TGNP

Katibu huyo wa Kituo, amesema kabla ya kuanzishwa kwa kituo hicho mwitikio wa jamii kushiriki shughuli za maendeleo ulikuwa mdogo lakini baada ya Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) kufanya uraghibishi na kuwawezesha kuanzisha Kituo, baadaye kuendesha midahalo  ya Bunge la jamii, wananchi walielekeza mijadala kwenye uhaba wa miundombinu kwenye sekta za elimu na afya, ambapo waliafikiana na kuweka mikakati ya kutatua changamoto hizo kwa haraka ili kuweka mazingira mazuri katika upatikanaji wa elimu.

 “ wakati wa uraghibishi tuliziibua changamoto zilizokuwa zinakikabili kata yetu ambapo wananchi waliazimia kujenga nyumba ya mwalimu ambaye alikuwa anaishi katika moja ya Ofisi katika Shule ya Msingi Miyuguyu kutokana na uhaba wa makazi ya walimu,”amesema Kwilasa.

Naye Hamis Mashauri Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho amesema tatizo la uhaba wa nyumba za walimu katika shule ya Msingi Miyuguyu linasababisha walimu kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo ndio maana wanakijiji walihamasika na kuamua kujenga nyumba hiyo ili kuboresha mazingira bora ya kufanyia kazi.



“Shule hii inawanafunzi 524, madarasa sita, walimu wapo sita na nyumba za walimu zipo tatu mbili zizojengwa na serikali na moja iliyojengwa na wananchi baada ya Bunge la Jamii, mwalimu wa kike yupo mmoja tu na inauhaba wa walimu 11,”amesema Mashauri.

Mwezeshaji kutoka TGNP, Deogratius Temba,  akiwaeleza wanajamii wa Kijiji cha Miyuguyu, Kata ya Kiloleli, umuhimu wa kuendelea kushirikiana na viongozi na kuhamasishana kushiriki kwenye shughuli za maendeleo


Kwa upande wake Getrude Missana Mwalimu wa shule ya Msingi Miyuguyu amesema awali kabla ya kujengewa nyumba hiyo alikuwa anaishi katika moja ya ofisi katika Shuleni hapo hali iliyokuwa inamuwia vigumu kutekeleza majukumu yake hadi alipohamia katika nyumba iliyojengwa na wakazi wa kijiji hicho.

Wazee wa Kijiji hicho wakiwa kwenye vikundi vya majadiliano wakati wa tathimini. 

“Tunaiomba serikali ituboreshe mazingira ya kazi ikiwemo ujenzi wa Makazi ya walimu katika vituo vya kazi ili kutimiza majukumu yetu ipasavyo,hapa mimi ni mwalimu wa kike peke yangu niliyesalia wengi wakipangiwa wanaomba uhamisho kutokana na changamoto hizi,”amesema Missana.

Diwani wa kata hiyo, Edward Manyama, aliishukuru TGNP kwa kuwajengea uwezo wananchi wa kata hiyo na kujitambua hasa kuwa na moyo wa kujitoa katika shughuli za maendeleo.

Nyumba iliyojengwa na wananchi ili kumtoa mwalimu asiendelee kuishi kwenye darasa la shule hiyo , ambapo alikuwa akiishi na kukosa uhuru wa kutekeleza wajibu wake kikamilifu


Alisema kwamba, pamoja na Halmashauri kuanza  kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wakazi wa kijiji cha Miyuguyu na vijiji vingine ikiwemo ya walimu ambapo kwa sasa shule hiyo inakabiliwa na uhaba wa walimu 11 na waliopo ni sita pekee, bado nguvu ya jamii katika kushiriki kwenye shughuli za maendeleo inahitajika sana.

Nyumba iliyojengwa na wananchi ili kumtoa mwalimu asiendelee kuishi kwenye darasa la shule hiyo , ambapo alikuwa akiishi na kukosa uhuru wa kutekeleza wajibu wake kikamilifu


“Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kishapu imeahidi kuleta walimu wapya katika Shule ya Msingi Miyuguyu,niwaombe wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwao ili waweze kutimiza majumu ya kuwafundisha watoto wetu,”amesema Manyama.

Awali akizungumza wajumbe wa Kituo cha Taarifa na Maarifa  cha Kata ya Kiloleli kwenye Kijiji cha Miyuguyu Mwezeshaji kutoka TGNP, Deogratius Temba,  alipongeza jitihada zizofanikisha kujengwa kwa nyumba ya mwalimu ambaye awali alikuwa akiishi kwenye darasa mojawapo shuleni hapo.

“TGNP inawajengea uwezo wananchi kupitia vituo hivi ili waweze kuibua changamoto zinazowakabili na kuzipatia suluhisho wenyewe kwa kushirikiana na viongozi wao, ujenzi wa nyumba hii na matundu ya vyoo 12 ni kielelezo kwamba Wakazi wa kijiji cha Miyuguyu wamebadilika na wameamua kushiriki katika shughuli za maendeleo kwa pamoja,”amesema Temba na kuongeza:

“ sio hii tu, wakazi wa Kata hii kupitia Bunge la Jamii wamefanikiwa kujenga matundu 24 ya vyoo katika shule ya msingi Kiloleli, ambapo choo cha awali cha wnaafunzi kilikuwa kimejaa kabisa na kutitia, Bunge la Jamii lilipofanyika pale shuleni, kila mwanajamii alitakiwa kuangalia kile choo na kupendekeza jambo la

Mwisho.

No comments:

Post a Comment