Taifa la Tanzania linapata kiongozi, Baba wa kiroho na mshauri wa Papa kwa wakati mwingine, Watu wa Mungu wanamuombea matashi mema Katika utume wake nchini na Duniani.
![]() |
Mtangulizi, Kadinali wa Kwanza Mwafrika na Mtazania, Marehemu Mwadhama Laurian Rugambwa |
![]() |
Kadinal wa Pili Mtanzania kwa Taifa la Tanzania, na Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es saalam, Mwadhama Policarp Kadinal Pengo. |
Kardinali ni cheo kimojawapo cha juu katika Kanisa Katoliki, hasa Kanisa la Kilatini, lakini si daraja takatifu Ndio wanaomchagua Papa (Baba Mtakatifu)
Mkutano wa makardinali ndio
humchagua Papa mpya
ambaye ni mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani ambalo ndilo dhehebu la Ukristo kubwa kuliko yote.
Uchaguzi hutokea
baada ya Papa aliyetangulia kufariki au kung'atuka. Kwa mara ya kwanza kwa
historia ya Kanisa, Marehemu Papa Benedict ndiye aliomba kustaafu katika kiti
na kumwachia Papa Francis. Lakini
kardinali aliyefikia umri wa miaka 80 hashiriki tena katika uchaguzi wa Papa.
Kati ya kifo cha Papa na uchaguzi wa mwandamizi wake ni
mkutano wa makardinali unaoongoza Kanisa lote kwa muda.
Uteuzi wa kardinali mpya
Kwa kawaida kardinali huteuliwa kati ya maaskofu, lakini kuna pia makasisi wachache wanaoteuliwa na Papa kuwa kardinali bila kupewa uaskofu.
Mwenye kuteua makardinali ni Papa peke yake, naye ana haki ya kumteua kardinali hata bila kutangaza jina lake hadharani (yaani anakuwa kardinali kwa siri). Kardinali ya aina hiyo huitwa kwa Kilatini "in pectore" (yaani "moyoni"). Hii inaweza kutokea hasa kama ni kardinali kutoka nchi pasipo uhuru wa dini au nchi ambayo haina uhusiano mzuri na Kanisa Katoliki
Wajibu wa makardinalI
Wajibu mkubwa ni kumchagua mwandamizi wa Papa, lakini pia ni kazi yao kumshauri katika kuongoza Kanisa lote.
Kwa kawaida viongozi wa idara kadhaa za
Kanisa wanapewa kofia ya
kardinali.
Pia kwa sababu hiyo kuna idadi ya makardinali wanaoishi Vatikani au katika mitaa mingine ya jiji la Roma maana yake hawana majimbo au hawapo majimboni kama alivyokuwa Mwadhama Pengo.
Hata hivyo kwa sasa wengine wengi wanaishi katika nchi mbalimbali, wakiongoza majimbo. Hiyo haina maana kwamba wao ni wakuu wa maaskofu wenzao wa nchi hiyo au kwamba wana mamlaka yoyote juu ya Kanisa la nchi hizo.
Idadi ya makardinali
Hakuna idadi maalumu ya makardinali na mnamo 7 Novemba 2021 walifikuwa 215.
Papa Paulo VI aliunda utaratibu kuwa
wasiwepo zaidi ya makardinali 120 wenye haki ya kupiga kura. Wale waliofikia
umri wa miaka 80 hawashiriki tena katika uchaguzi wa Papa mpya. Lakini
kardinali hajiuzulu wala kustaafu: anaendelea na cheo na pia na haki ya
kushiriki katika mkutano wa makardinali hadi kifo. Kardinali aliyestaafu kuwa
Askofu Jimbo au kuachia kiti cha Uaskofu Jimbo, anaendelea na majukumu kama
Askofu Mstaafu-Jimbo (Bishop Emeritus). Anaweza kuendelea kupangiwa majukumu kadiri
ya uwezo wake na Askofu Jimbo mahalia.
Kwa sababu ya uhusiano wao na Kanisa la Roma, kimapokeo makardinali wengi ni Waitalia, hata Mapapa walikuwa Waitalia watupu kwa karne nne mfululizo hadi alipochaguliwa Papa Yohane Paulo II, Mpolandi.
Lakini asilimia ya makardinali Waitalia imepungua: kabla
ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia zaidi ya
nusu walikuwa Waitalia, siku hizi hawafikii asilimia 25.
MAKALA HII IMEUNGANISHWA KUTOKA VYANZO MBALIMBALI NA KUHARIRIWA NA
Deogratius Temba, kwa msaada wa Mitandao.
0784686575